Zenj FM

Magofu, viwanja vyatumika kutupia taka Bububu Kigamboni

13 September 2024, 3:45 pm

Eneo la kiwanja kinacholalamikiwa kwa kutupia taka.

Na Mulkhat Mrisho Bushir,

Mwananchi wa shehia ya Bububu Kigamboni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja amelalamikia vitendo vya baadhi ya wananchi wanaotupa taka hovyo katika maeneo yasiyo rasmi hususani kwenye kiwanja  vilivyo wazi na magofu ya nyumba ambazo hazijaisha.

Akizungumza  na Zenji FM Bububu Kigamboni amesema  kuna baadhi ya wananchi wanaotupa takataka katika eneo hilo la kiwanja ambacho kipo karibu na nyumba yake  jambo ambalo linahatarisha usalama wa wakazi wa eneo hilo.

Aidha  mwananchi huyo ameiomba  serikali kupitia uongozi wa shehia  kumtafuta mwenye kiwanja hicho  ili kutatua changamoto ya utupwaji wa taka katika eneo hilo.

Sauti ya mwananchi.

Naye sheha wa shehia Bububu Kigamboni  Halima Twaha amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kuwataka wananchi wenye tabia hyo kuacha mara moja kwani  serikali  haitasita kuwachukulia  hatua  kali kila mwananchi atakayejihusisha na utupaji taka katika kiwanja hicho.