Zenj FM

Waislam watakiwa kutoa kipaumbele uhifadhi Quran kwa watoto

19 August 2024, 6:02 pm

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Alhaj Ayoub Mohd Mahmoud (aliyevaa kanzu nyeupe) akiwa na Wajumbe wa kamati  Kuu ya Jumuiya ya kuhifadhisha Qurani Zanzibar.

Na Mary Julius

Jumla ya wanafunzi 26 kutoka vyuo mbalimbali vya Wilaya ya  Kusini kiwemo Jambiani, Bwejuu, Paje, Muyuni, Makunduchi na Kizimkazi  wameshiriki katika   mashindano ya kuhifadhi Quran kwa wanafunzi wa  madrasa ambapo mshindi wa kwanza kwa upande wa wanawake ni Halima Amour Juma  kutoka  Kizimkazi Dimbani na kwa wanaume ni Maftah Hussein  Saleh kutoka  Jambiani Kibigija.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja  Alhaj Ayoub Mohd Mahmoud  amewasisitiza  waumini na viongozi wa dini ya kiislam kulipa kipaumbele Suala la kihifadhi Qurani kwa watoto  kwa lengo la jamii kuwa na vijana wenye madili  mema

Alhaji  Ayoub ametoa kauli hiyo katika msikiti wa skuli ya Sekondari Hasnuu Makame wakati  akifungua Mashindano ya kihifadhi Qurani kwa wanafunzi wa  madrasa kutoka  katika Maeneo mbali mbali ya Wilaya  ya Kusini  ikiwa ni muendelezo  Wa maashimisho ya siku ya Kizimkazi .

Amesema Suala la watoto kuhifadhi Qurani  ni jambo lenye faida kubwa  kwani linamkurubisha mja na mola wake  hivyo ni  Vyema  viongozi wa dini,wazazi na walimu  kuona umuhim wa kuliendeleza ili kuwajengea watoto kiimani  na dini yao Hali itayopelekea  pia kusaidia kupunguza mmongonyoko wa maadili.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja  Alhaj Ayoub Mohd Mahmoud. 

Kwa upande wao mjumbe wa kamati  Kuu ya Jumuiya ya kuhifadhisha Qurani Zanzibar Sheh Saleh Ali  na  Amiri kanda ya Kizimkazi   Sheh  Hassan Omar Khamis wamesema   kuendelezwa kwa matamasha ya  Ramadhan  na matamasha mengine yanayofungamana na masuala ya dini ya kiislam  kutasaidia  kukuza harakati za  uislamu  ndani ya mkoa   huo.

Sauti ya Wajumbe wa kamati  Kuu ya Jumuiya ya kuhifadhisha Qurani Zanzibar.

Nao wanafunzi walioshiriki katika mashindano hayo  wamewashukuru  viongozi wa nchi , wadini na wa madrasa kwa kuandaa  mashindano hayo  na kuwataka wanafunzi wenzao kushiriki katika mashindano hayo ambayo yanaleta manufaa hapa duniani na kesho akhera.

Sauti ya wanafunzi.