Zenj FM

Tamasha la Kizimkazi lawafikia wavuvi wilaya ya Kusini Unguja

16 August 2024, 3:42 pm

Waziri wa Uchumi wa Buluu na  Uvuvi Zanzibar Shaban  Ali Othman akifungua mafunzo ya siku Tano kwa  wavuvi kutoka Shehia  mbali mbali za wilaya ya kusini unguja.

Na Mary Julius.

Waziri wa Uchumi wa Buluu na  Uvuvi Zanzibar Shaban  Ali Othman amesema dhamira ya  Serekali zote mbili nchini  ni kuimarisha  Sekta ya uchumi wa bluu na kuona   wavuvi wanapata tija  na pato la taifa linaongezeka .

Waziri wa Uchumi wa Buluu na  Uvuvi Zanzibar Shaban  Ali Othman  amesema  serkali itaendelea kuchukua juhudi za  kuielimisha jamii  juu ya matumizi  na utunzaji wa rasilimali za  bahari  ili  ziweze kunufaisha  vizazi vya sasa na vjavyo

Akizungumza  huko Kizimkazi wakati akifungua mafunzo ya siku Tano kwa  wavuvi kutoka Shehia  mbali mbali za wilaya ya kusini   juu ya   namna  Bora na  salama ya Uhifadhi na uchakataji  wa samaki na mazao mengine ya bahari kiwa ni miongoni mwa  harakati  za kuelekea katika  madhimisho ya Tamasha la   siku ya  kizimkazi.  

Amesema hatua hiyo itasaidia  kuongeza kipato kwa wavuvi  na pia  kuondosha  matatizo  mbali mbali ikiwemo  ya uvuvi Haram na  migogoro ya wenyewe kwa wenyewe  Pamoja  na serikali inayojitokeza mara kwa mara.

Sauti ya Waziri wa Uchumi wa Buluu na  Uvuvi Zanzibar Shaban  Ali Othman.

Nae  Mkurugenzi   Mkuu Mamlaka ya Uvuvi Bahari Kuu  Tanzania Dk Immanuel  sweke   amesema serekali  imeona kuna umuhimu mkubwa  wa  kuandaa mafunzo hayo kwa wavuvi wadogo wadogo kutokana  na mchango wao mkubwa  wa  kuisaidia jamii  katika kupata Chakula na pia  kujiwezesha kiuchumi.

Sauti ya Mkurugenzi   Mkuu Mamlaka ya Uvuvi Bahari Kuu  Tanzania Dk Immanuel  Sweke

Nao wavuvi hao wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kufanya shughuli zao za uvuvi kwa uhakika na kuahidi kuisambaza elimu hiyo kwa wavuvi wengine.