Zenj FM

Vikundi Zanzibar vya tahadharishwa mikopo ya riba

7 August 2024, 5:01 pm

Mkurugenzi Wa Idara Ya Maendeleo Jamii, Jinsia Na Watoto, Siti Abasi Ali akizungumza na wenyeviti, makatibu na washika fedha wa vikundi vya wilaya ya mjini.

Na Steven Msigaro.

Wanawake  wajasiriamali wametakiwa  kuacha kuchukua mikopo yenye riba kubwa na badala yake wachukua mikopo  inayo tolewa na serikali.

Mkurugenzi Wa Idara Ya Maendeleo Jamii, Jinsia Na Watoto. Siti Abasi Ali ameahidi kusaidia  vikundi vya wanawake wajasiriamali kuweza kupata mkopo isiyo na riba inayotolewa  na Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.

Akizungumza na wenyeviti, makatibu na washika fedha wa vikundi vya wilaya ya mjini huko seblen kwa wazee, mkurugenzi amesema mikopo yenye riba imekuwa kikwazo kikubwa kwa wajasiriamali katika kujikomboa kiuchumi hivyo kwa kuliona hilo serikali kwa kupitia  fedha za uviko 19, halmashauri na manispaa kupitia uwezeshaji, imeweza kutoa mikopo isiyo na riba.

Aidha Mkurugenzi amevitaka vikundi visivyosajiliwa kupitia waratibu kuhakikisha vinasajiliwa kuepukana na changamoto za kukosa mikopo inayotolewa  na Serikali.

Sauti ya Mkurugenzi Wa Idara Ya Maendeleo Jamii, Jinsia Na Watoto, Siti Abasi Ali.

Kwa upande wao wanavikundi wamesema mchakato mrefu wa upatikanaji wa mikopo ya serikali ndio unaosababisha wajasiriamali wengi kuachana na maombi ya mikopo hiyo na kuangukia kwenye mikopo yenye riba kubwa  na kupata hasara.

Sauti ya wanavikundi.