Zenj FM

Udongo sababu ya ucheleweshaji wa mradi wa ujenzi wa barabara Pemba

30 July 2024, 2:45 pm

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na wananchi wa Mzambarau Takao mara baada ya kukagua ujenzi wa mradi wa soko la samaki na mboga mboga linalijengwa katika eneo hilo akiwa katika ziara zake za kukagua miradi ya maendeleo inayojengwa Kisiwani Pemba.

Na Mary Julius.

Kampuni ya MECCO imetoa sababu za mradi wa ujenzi wa barabara ya chakechake/wete kuchelewa utekelezaji wake baada ya kubainika udongo wa barabara ya zamani unahitaji kuchimbwa na kuondolewa udongo kabla ya kuweka udongo mwingine na kusababisha ukubwa wa kazi kuongezeka.

Hayo yameelezwa na Muhandisi wa Kampuni hiyo Nassor Ramadhan wakati akitoa taarifa za maendeleo ya ujenzi huo kwa makamu wa pili wa rais alipokagua ujenzi wa mradi huo kisiwani Pemba.

Sauti ya Muhandisi wa Kampuni MECCO Nassor Ramadhan

Kwa upande wake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amewataka wasimamizi wa mradi huo kuongeza kasi ya ujenzi kwa vile barabara hiyo inaumuhimu mkubwa kiuchumi kwa wananchi kisiwani Pemba.

Sauti ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla.

Naye Waziri wa Mawasiliano,Usaifirishaji na Uchukukuzi Dk Khalid Salum Muhamed amesema itakuwa vizuri mradi huo ukamilike kwa wakati ili kuzinduliwa januari mwakani.

Sauti ya Waziri wa Mawasiliano Usafirishaji na Uchukukuzi Dk Khalid Salum Muhamed.

Hata hivyo taarifa za ndani zinasema mradi huo umekuwa katika mazingira magumu baada ya mkandarasi kutolipwa kwa wakati malipo namba nne baada ya kuchelewa kwa siku 177 zaidi ya miezi sita na kulazimika kuchukua mkopo wa shilingi bilioni saba benki ili kuendeleza mradi huo.