Zenj FM

Wanawake wahimizwa kuchangamkia fursa za mikopo nafuu

4 July 2024, 5:22 pm

Mjumbe wa Halmashauri kuu Taifa Mkoa wa Mjini Asya Ali Khamis akifungua baraza kuu la umoja wa Wanawake Tanzania uwt mkoa wa kusini unguja lililofanyika Dunga Wilaya ya Kati.

Na Ahmed Abdulla

Wajumbe wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wanawake Tanzania UWT mkoa wa Kusini Unguja wamehimizwa kuwashajihisha wanawake na vijana kujiunga katika vikundi vya ushirika na kuchukua mikopo nafuu inayotolewa na serekali ili waweze kujiwezesha kiuchumi

Akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza Kuu la Jumuiya ya Wanawake Tanzania UWT Mkoa wa Kusini Unguja, ukumbi wa Walimu Dunga  mjumbe wa  Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa Kutoka Mkoa wa Mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza kuu la UWT Taifa, Asya  Ali Khamis amesema hatua hiyo itayasaidia makundi hayo kuondokana na mikopo yenye riba kubwa ambayo inarejesha nyuma juhudi zao za kuwaketea maendeleo.

Akizungumzia kuhusu sula udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto Asya ameitaka jamii kuzingatia umuhimu wakurejesha utamaduni wa malezi ya pamoja  kwa lengo la kupata watoto wenye maadili mema na watakaoweza kulitumikia vyema taifa katika nyanja mbali mbali za kijamii na kiuchumi.

Sauti ya Mjumbe wa  Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa Kutoka Mkoa wa Mjini Asya  Ali Khamis.

Nae Mwenyekiti wa Umoja Huo mkoani Humo Shemsa Abdalla Ali amewasisitiza wajumbe kuendelea kuulinda mkoa wa Kusini ili ubaki kuwa Ngome ya Chama Cha Mapinduzi.

Sauti ya Mwenyekiti wa Umoja Huo mkoani Humo Shemsa Abdalla Ali

Nao baadhi ya wajumbe wa baraza hilo wameiomba serikali kuimarisha uharaka wa utoaji wa mikopo kwa akinamama ili kufikia wanawake wengi.

Sauti ya baadhi ya wajumbe wa baraza hilo.

Katika baraza hilo mwakilishi wa viti maalumu mkoa wa Kusini Unguja nafasi za watu wenye ulemavu Mwantatu Khamis Mbaraka amekabidhi kadi 1,500 za jumuiya hiyo kwa wilaya ya Kusini na Wilaya ya Kati.