Zenj FM

Mwakilishi atekeleza ilani kwa vitendo Chumbuni

3 June 2024, 5:41 pm

Mwakilishi wa jimbo la Chumbuni akikabidhi tank, mpira wa maji na pampu ya maji kwa Mwenyekiti wa Tawi la Mwembe makumbi b. Picha na Mary Julius.

Na Mary Julius

Wakazi wa shehia  mwembe makumbi kwa muda mrefu wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama katika shehia hiyo hali iliyo sababisha mwakilishi wa jimbo la chumbuni kuwachimbia kisima katika eneo lao.

Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Miraji Khamis Kwanza amekabidhi  tanki  la maji lenye ujazo wa miilis 5000 pamoja na  pampu na mipira kwa ajili ya usambazaji  wa maji safi na salama kwa wakazi wa Mwembe makumbi ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo mwalikilishi amewaomba wakazi wa shehia hiyo kukitunza  na kukilinda kisima hiicho pamoja na vifaa ili viweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu.

Sauti ya Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Miraji Khamis Kwanza.

Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo Mwenyekiti wa Tawi la Mwembe makumbi b Bakari Mohammed Abdallah  amesema kutokana na harakati za utengenezaji wa barabara katika shehia hiyo mabomba mengi ya maji  yamekatwa na kusababisha ukosefu wa maji hivyio ujio wa kisima hicho kimekuwa mkombozi kwa wakazi wa eneo hilo

Aidha amempongeza Mwakilishi Miraji Kwanza kwa kuweza kutekeleza ombi hilo la kushimba kisima katika eneo hilo kwa haraka na kuahidi kukitunza pamoja na kulinda miundo mbinu ya kisima hicho.

Sauti ya Mwenyekiti wa Tawi la Mwembe makumbi b Bakari Mohammed Abdallah.