Zenj FM

Mwakilishi Chumbuni atimiza ahadi

31 May 2024, 4:21 pm

Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Miraji Khamis Kwanza akiwa katika ziara ya kukagua mtaro wa maji machafu eneo la Mwembe Makumbi. Picha na Mary

Na Mary Julius.

Shilingi milioni nane zinatarajia kutumika katika ujenzi wa mtaro wa maji machafu katika shahia ya Mwembe makumbi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa mtaro ambao umekatika na kusababisha mvua ikinyesha maji machafu kuingia katika nyumba za wakazi wa eneo hilo Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Miraji Khamis Kwanza amesema ujenzi wa mtaro huo utasaidia kuwaondolea wananchi wa eneo hilo changamoto walizokuwa wanakutana nazo hasa katika kipindi cha mvua.

Aidha wakilishi amewaomba wakazi waeneo hilo kutoa  ushirikiano katika kuhakikisha mtaro huo unajengwa.

Sauti ya Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Miraji Khamis Kwanza

Kwa upande wao Wananchi wa shehia ya mwembe makumbi wamemshukuru mwakilishi wa jimbo la chumbuni kwa kuwaletea vifaa hivyo  ambapo wamesema kupasuka kwa mtaro huo kumepelekea kipindi cha mvua  maji kuingia katika nyumba zao na kuhatarisha afya za wakazi wa eneo hilo.

Aidha wananchi wamesema mtaro huo ambao juu upo wazi umekuwa ukihatarisha maisha ya watoto wadogo na watu wazima wanaoishi katika eneo hilo. 

Sauti ya w