Zenj FM

Mvua yaathiri uzoaji taka Wilaya ya Magharib A

1 May 2024, 7:28 pm

Sehemu ya taka zilizoto katika eneo la Bububu meli nane. Picha na suleiman.

Na Rahma na Suleiman

Mkusanyiko wa taka kwa muda mrefu wawaibua wakazi wa Bububu meli nane.

Wananchi wa Bububu meli nane wadi ya kihinani wilaya ya magharibi( A)  mkoa  wa mjini wameilalamikia  Manispaa ya wilaya hiyo kuwepo  kwa taka  muda mrefu .

 Wakizungumza na zenji fm wananchi hao wamesema kukithiri kwa taka hizo  kunahatarisha maisha ya wakaazi na wapita njia wa eneo hilo,

Aidha wamesema mkusanyiko huo unapelekea maradhi ya mripuko hususani katika kipindi hichi cha mvua zinazoendelea kunyesha, wamaeiomba mamlaka husika kulitafutia ufumbuzi suala hilo

Sauti ya wananchi.

Diwani wa wadi ya kihinani Nyange Hajji amekili kuwepo kwa changamoto ya taka katika eneo hilo  amewaomba  wananchi wa bububu meli nane kuwa na subra katika kipindi hiki kigumu wanachokipitia.

Sauti ya Diwani wa wadi ya kihinani Nyange Hajji.

Akithibitisha kuwepo kwa changamoto hiyo Mkuu wa Idara Huduma za Jamii Mazingira na Mipango Miji Baraza la Manispaa Magharibi (A) Tatu Hussen Abdalla amesema changamoto kubwa ya kukaa taka hizo kwa muda mrefu ni mvua kubwa za elnino zinazoendelea kunyesha hapa nchini.

Sauti ya Mkuu wa Idara Huduma za Jamii Mazingira na Mipango Miji Baraza la Manispaa Magharibi (A) Tatu Hussen Abdalla