Keifo FM

walimu walishwa cake na wahitimu

6 February 2026, 17:57

picha na emmanuel jotham. Mwalimu mkuu wa keifo sekondary akilishwa keki na mhitimu wa kujitegemea

katika tukio lisilo la kawaida wahitimu wa kujitegemea katika shule ya sekondari keifo wameamua kununua keki na soda na kuwapelekea walimu kwa ajili ya kuwapongeza baada ya kuwawezesha kupata ufaulu mzuri katika masomo yao

Na Emmanuel jotham

Wahitimu wa kujitegema wali hitimu kidato cha nne katika shule ya secondary keifo iliyopo wilayani kyela mkoani Mbeya wamewapongeza walimu wa shule hiyo kwa kwasaidia wahitimu hao kufaualu masomo yao kwa kiwango cha juu.

picha ya pamoja walimu na wahitimu katika jengo la utawala keifo sekondari

Hatua hiyo ya kuwapongeza walimu   wa   shule hiyo imekuja baada ya wao kama wahitimu wa kujitegema yaan PC Kupewa ushirikiano wa hali ya juu pindi walipo kuwa shuleni hapo kwa miezi 9 na kuepeka wao kufaulu masomo yao.

Wakizungumza kwa furaha kubwa wahitimu hao wa kujitegemea wamesema wamemaua kununua cake na soda na kufurahi Pamoja na walimu hao  kama alama ya ushindi katika safari yao ya elimu.

sauti ya wahitimu wa keifo sekondari

Awali akiwakaribisha katika tukio hilo la kupongezana mkuu wa shule ya sekondari keifo mwl skoti amesema kitendo walicho kifanya wahitimu hao kinaongeza motisha kubwa kwa walimu na kuwafanya waongeze bidi katika ufundishaji.

sauti ya mkuu wa keifo sekondari

Kwa upande  wao walimu wa shule ya sekondari keifo wamepongeza hatua ya wahitimu hao kwa kuwajali  walimu walio wafundisha na kuwatakia kila rhahel kuelekea hatua inayo fuata katika safari ya elimu.

sauti ya walimu wa keifo sekondari

Shule  ya keifo sekondari ni shule ya binafsi inayo patika wilayani kyela kata ya Serengeti ambayo inajumuisha wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka kidato cha sita .

jengo la utawala keifo sekondari