Keifo FM

Kyela:Kyela yang’ara ukusanyaji mapato robo ya pili

7 February 2025, 16:35

Pichani ni viongozi wa halmashauri ya wilaya ya kyela wakati wa baraza la robo ya pili lililofanyika katika ukumbi wa mikutano kyela picha na James Mwakyembe

Serikali ya halmashauri ya wilaya ya Kyela imewapongeza wananchi kwa kuwezesha halmashauri kukusanya asilimia 98 za makusanyo kutoka katika vyanzo vyake.

Na James Mwakyembe

Baraza la madiwani la robo ya pili ya Mwaka la mrejesho kwa wananchi juu ya kipi kimefanyika limefanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya kyela huku halmashauri ikivunja rekodi ya ukusanyaji mapato kwa kusanya jumla ya asilimia 98 ambayo haijawahi kutokea katika historia ya kyela.

Akifungua baraza hilo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kyela ambaye pia ni diwani wa kata ya Ikimba Katule Kingamkono amesema katika kipindi hicho serikali ya awamu ya sita imetoa fedha jumla ya shilingi bilioni moja nukta tano kwa ajiri ya kumalizia jengo la mama na mtoto katika hospitali ya wilaya ya Kyela.

Sauti katule kuhusu za jengo la mama na mtoto

Akitoa taarifa ya hali ya ukusanyaji wa mapato katika robo hii ya pili ya mwaka katule amesema halmashauri imeweza kukusanya mapato kwa silimia 98 katika robo ya pili jambo ambalo amekiri kuwa halijawahi kutokea katika wilaya ya kyela pamoja kuwashukuru mkurugenzi na watalaamu wote pamoja na wananchi kwa kutambua umuhimu wa kutoa kodi.

Sauti ya katule kuhusu kuvunja rekodi ya ukusanyaji mapato
Pichani ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kyela Katule Kingamkono wakati wa baraza la madiwani la robo ya pili.

Pia Katule amezungumzia hali ya nidhamu kazini huku akibainisha kuwa jumla wa watendaji wawili wamefukuzwa kazi pamoja na kumshusha kiwango cha mshahara mtumishi mmoja baada ya kubainika kuwa na makosa ya kiutendaji kazini.

Sauti ya katule kuhusu kuwafuta kazi watendaji wasio waadirifu.
Pichani ni madiwani pamoja na wageni waalikwa wliohudhulia baraza la madiwani la robo ya pili katika ukumbi wa halmashauri ya Kyela

Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya kyela limeketi ikiwa ni utaratibu ulijiwekea kwaajiri ya kutoa mrejesho wa taarifa mbalimbali kwa wananchi wake juu ya namna mambo mbalimbali ya kimaendeleo yanavyotekelezwa na viongozi waliowapa dhamana ya kuwaongoza katika kata zao.