Keifo FM

Kilele cha wiki ya sheria chafanyika kwa kishindo Kyela

4 February 2025, 19:17

Pichani baadhi ya wadau walioshiriki katika kilele cha wiki ya sheria wakiwa na hakimu mkazi mkuu mfawidhi pamoja na mkuu wa wilaya ya kyela na Nsangatii Mwakipesile

Mamia ya wananchi wamejitokeza katika viwanja vya mahakama ya wilaya ya kyela kusikiliza na kuwasilisha kero zao zilizotatuliwa na jopo la watalaamu wa sheria katika kilele cha wiki ya sheria hapa wilayani kyela.

Na Nsangatii  Mwakipesile

Hatimaye kilele cha wiki ya sheria hapa wilayani kyela kimefanyika leo huku mkuu wa wilaya ya kyela Josphin Manase  akiwapongeza viongozi na wafanyakazi wa  Mahakama kwa kazi kubwa ya kushughulikia ipasavyo malalamiko ya wananchi na kuwasii kuendelea kutenda haki kwa muujibu wa sheria.

Akizungumza mbele ya wafanyakazi na wananchi walio jitokeza kwenye sherehe hizo Manase amewapongeza wafanyakazi kwa kupunguza msongamano wa kesi nyingi Mahakamani tofauti nah apo awali hivyo kuwaomba kuendelea kusimamia haki kikamilifu kwa kufuata misingi ya taaluma yao.

sauti ya mkuu wa wilaya ya kyela akizungumza kuhusu mahakama kufanya vizuri
Mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Kyela Josephine Manase akihutubia katika kilele cha wiki ya sheria viunga vya mahakama ya wilaya kyela

Katika hatua nyingine Manase amesema ni vema mahakama ikaon umuhimu wa kupeleka huduma za kisheria kwa wananchi kwenye kata zao ili kuwasogeza elimu Pamoja na kuwatatulia migogoro ihusuyo sheria katika maeneo yao.

sauti ya mkuu wilaya kyela kuhusu mahakama kusogeza huduma katika kata zote

Nae         Hakimu mkazi mkuu  mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kyela Andrew Severin Njau amewashukuru wadau na wananchi wote walioshiriki kwenye maadhimisho hayo na kuahidi kuyafanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolwa na mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa wilaya ya kyela.

Pichani ni Hakimu mkazi mkuu  mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kyela Andrew Severin Njau akiwa na mkuu wa wilaya ya Kyela Josephine Manase

Madhimisho haya ya wiki ya sheria hufanyika kila mwaka ikiwa ni sehemu ya utambulisho wa shughuli mpya za mwaka wa mahakama ambazo hutanguliwa kwa kutoa elimu ambapo wadau wa sheria huzunguka katika kada mbalimbali kutoa elimu ihusuyo sheria hapa nchini.