Karagwe FM

CBIDO yatoa msaada wa mashine ya mionzi Missenyi

26 September 2025, 11:37 am

Meneja miradi wa shirika la CBIDO Bw. Donatus Kaihura (kushoto) akikabidhi mashine ya ultra sound kwa Kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya Missenyi Dkt Jamil Yahya (kulia)

Shirika la CBIDO lenye makao makuu yake wilayani Karagwe limeendelea na mradi wake wa Pamoja unaolenga kuzuia ulemavu na kutoa huduma za utengamao kwa watu wenye ulemavu kwa kata za Kyaka na Kilimilile Wilayani Missenyi mkoani Kagera na mara hii likitoa msaada wa vifaa tiba

Na Respicius John, Missenyi, Kagera

Zahanati za Kyaka na Kilimilile zilizoko wilayani Missenyi zimepokea msaada wa mashine ya mionzi ultra sound kutoka shirika la CBIDO la Karagwe itakayosaidia kuchunguza wanawake wajawazito ili kudhibiti ulemavu kwa watoto kabla ya kuzaliwa

Kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya Missenyi Dkt Jamil Yahya. Picha na Respicius John

Akikabidhi mashine na kitanda chake vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 14 meneja miradi wa shirika la CBIDO Bw. Donatus Kaihura amesema kuwa mashine hiyo imetolewa kama sehemu ya utekeleza wa mradi wa kuzuia ulemavu na kutoa huduma za utengamao ambapo kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya Missenyi Dkt Jamil Yahya ametoa shukurani kwa shirika hilo

Meneja miradi wa shirika la CBIDO Bw. Donatus Kaihura na Kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya Missenyi Dkt Jamil Yahya

Nao baadhi ya wataalam wa afya katika zahanati za Kilimilile na Kyaka wamesema kuwa mashine hizo zitasaidia pakubwa katika kupunguza matatizo ya uzazi kwa wananchi

Baadhi ya wataalam wa afya katika zahanati za Kilimilile na Kyaka

Baadhi ya wanufaika wa kike na kiume wameeleza kufurahishwa kwao na msaada huo kwenye maeneo yao wakisema kuwa kimesaidia kurahisha huduma za uzazi

Baadhi ya wananchi watakanufaika na msaada huo