Karagwe FM

Vijana Kagera watakiwa kutoshawishiwa kuvuruga uchaguzi

26 May 2025, 7:12 pm

Mkurugenzi wa taasisi ya mabalozi wa amani Tanzania PPA Bw. Maulid Rashidi Kambuga. Picha na Theophilida Felician

Vijana mkoani Kagera wameaswa kukaa kando na makundi ya kisiasa yanayotumia kundi hilo kuleta vurugu nyakati za uchaguzi

Na, Theophilida Felician, Bukoba.

Kuelekea uchaguzi mkuu vijana mkoani Kagera na Tanzania kwa ujumla wametakiwa kuwa makini na watu wenye nia ya kuwashawishi kushiriki matendo ya vurugu za kuhatarisha amani ya nchi.

Wito huo umetolewa na viongozi wa taasisi ya mabalozi wa amani Tanzania PPA yenye makao yake manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Wakizungumza na vyombo vya habari viongozi hao wamefafanua kuwa nyakati kama hizi kundi la vijana huonekana kama kundi muhimu hivyo hujikuta wakitumiwa na watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa kwa malengo ya kuwavusha katika harakati zao za kisiasa na wengine huwatumia ndivyo sivyo hali inayosababisha kuwepo kwa matukio ya vurugu

Maulid Rashidi Kambuga ni mkurugenzi wa taasisi hiyo ambaye amesema amani ikishatoweka hakuna pa kukimbilia iwe kwa vijana, wazee, akina mama, watoto wote wanaathirika.

Mkurugenzi wa taasisi ya mabalozi wa amani Tanzania PPA Bw. Maulid Rashidi Kambuga
Mkurugenzi msaidizi wa PPA Mchungaji Clavery Venant. Picha na Theophilida Felician

Naye Mchungaji Clavery Venant ambaye ni mkurugenzi msaidizi wa PPA amebainisha kuwa kundi la vijana hawana budi kuishi kwa hofu ya Mungu na kuzingatia misingi ya maadili mema huku Bahati Ildephonce ambaye ni mkazi wa Bukoba yeye akieleza kuwa amani ikishavunjika husababisha madhara mengi kwa jamii

Mchungaji Clavery Venant pamoja na Bahati Ildephonce
Viongozi wa PPA wakizungumza na wanahabari. Picha na Theophilida Felician

Kwa pamoja wametoa wito kwa wananchi kuwa wazalendo wa kweli ili kulinda na kujenga Tanzania ya amani kwani