Karagwe FM

Vibanda 10 vya wafanyabiashara vyateketea kwa moto Bunazi Missenyi

18 February 2025, 8:06 pm

Sehemu ya vibanda vya wafanyabiashara vilivyoteketea kwa moto. Picha na Respicius John

Wafanyabiashara na wajasiriamali nchini wameendelea kukumbwa na hasara za mara kwa mara kutokana na moto unaoripuka katika maeneo yao ya kazi kutokana na uhaba wa miundombinu rafiki ya uzimaji moto pindi unapotokea

Na Respicius John

Wafanyabiashara katika mji mdogo wa Bunazi wilayani Missenyi wamepata hasara baada ya moto kuteketeza jumla ya vibanda kumi pamoja na mali zote zilizokuwemo ambazo thamani yake haijajulikana

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kitongoji cha Kashozi B kata ya Kasambya wilayani Missenyi Mwl. Ruchius Bukambu vibanda hivyo viliunguzwa na moto ulioripuka usiku wa kuamkia Februari 17.2025

Sauti ya mwenyekiti wa kitongoji cha Kashozi B kata ya Kasambya wilayani Missenyi Mwl. Ruchius Bukambu
Eneo la vibanda vya wafanyabiashara wa Bunazi lililokumbwa na moto na kila kilichokuwepo kuteketea. Picha na Respicius John

Mmoja wa wafanyabiashara waliokuwa na vibanda katika eneo hilo bi Edina Josia amesema kuwa alipokea simu ya saa 7:30 usiku akitaarifiwa kuungua kwa eneo la biashara zao na kwamba alipofika alikuta kila kitu kikiwa kimeteketea huku mashuhuda wakisema kuwa huenda moto huo ulitokana na hitilafu ya umeme

Mmoja wa waathiriwa wa moto kwenye vibanda bi Edina Josia pamoja na mashuhuda

Hata hivyo kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Kagera Joseph Ngonyani amesema kuwa chanzo cha moto bado kinachunguzwa na kwamba hakuna madhara ya kibinadamu yaliyojitokeza

Kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Kagera Joseph Ngonyani