Karagwe FM

Vijana watakiwa kushiriki mapambano ya rushwa Missenyi

1 June 2024, 6:42 pm

Mkuu wa wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga (mwenye suti katikati) akiwa katika tamasha la klabu za vijana wapinga rushwa wilayani humo.Picha na Respicius John

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU nchini imeendelea na kampeni za kudhibiti vitendo vya kutoa na kupokea rushwa kwa kutumia makundi ya vijana katika shule za sekondari maarufu kama klabu za wapinga rushwa

Na Respicius John

Vijana wanaoendelea na masomo katika shule mbalimbali za sekondari wilayani Missenyi mkoani Kagera wametakiwa kushirikiana na jamii katika vita dhidi ya rushwa na biashara ya dawa za kulevya ili kuweka mazingira bora ya upatikanaji wa haki.

Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya ya Missenyi mkoani Kagera kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga katika tamasha la klabu za vijana wapinga rushwa kutoka shule mbalimbali za sekondari wilayani humo lililofanyika katika uwanja wa mashujaa Bunazi na kueleza kuwa vitendo vya rushwa hudumaza haki za watu na kuongeza mzunguko wa biashara ya dawa za kulevya kwa vijana wenye tamaa ya mali

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga
Mkuu wa wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga (wa kwanza kushoto) akiwa na baadhi ya maafisa wa TAKUKURU, Uhamiaji na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ngazi ya wilaya. Picha na Respicius John

Akiongea kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Missenyi mkuu wa divisheni ya kilimo, mifugo na uvuvi bi Tapita Tuvana Solomoni ameipongeza taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini TAKUKURU kwa kutoa mafunzo kwa vijana juu ya madhara ya rushwa akisema kuwa kufanya hivyo kutaokoa kizazi kijacho ambapo hata hivyo vijana walitaja baadhi ya madhara ya rushwa katika jamii

Sauti ya kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Missenyi bi Tapita Tuvana Solomoni pamoja na baadhi ya vijana kutoka klabu za wapinga rushwa
Baadhi ya vijana kutoka katika klabu za wapinga rushwa wilayani Missenyi. Picha na Respicius John

Tamasha la klabu za wapinga rushwa wilayani Missenyi limeratibiwa na TAKUKURU wilayani humo ambapo afisa wa taasisi hiyo bw. Sospeter Joseph amewataka wananchi wote kutoa ushirikiano TAKUKURU ili kuiwezesha kupambana na rushwa katika jamii

Sauti ya afisa wa TAKUKURU wilaya ya Missenyi bw. Sospeter Joseph