Zenj FM

Mdahalo wa ‘uchaguzi bila vurugu’ wasisitiza ushirikiano na utulivu

17 October 2025, 6:26 pm

Mkurugenzi wa Pamoja Youth Initiative Rashid Mwinyi wa katikati Mkurugenzi wa idara ya maendeleo ya vijana Zanzibar Shaibu Ibrahim Mohammed wa mwisho mkuu wa kurugenzi ya huduma za uchaguzi Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC Khamis Issa Khamis.

Na Berema Suleiman Nassor.

Mkurugenzi wa Idara ya  Maendeleo  ya Vijana Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Shaibu Ibrahim Mohammed amewataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kudumisha amani na utulivu  wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Akizungumza katika mdahalo wa  uchaguzi bila ya vurugu ulioandaliwa na taasisi ya Pamoja Youth Initiative amesema mdahalo huo si mkutano tu bali ni juhudi za kutunza Amani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kupitia uelewa na ushirikiano katika kuhakikisha uchaguzi wa mwaka 2025  unakuwa wa Amani  umoja  na ukomavu wa kidemokrasia.

Sauti ya Mkurugenzi wa Idara ya  Maendeleo  ya Vijana Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Shaibu Ibrahim Mohammed.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa tasisi ya Pamoja Youth Initiative Rashid Mwinyi amesema malengo ya mdahalo huo ni kuimarisha  ushirikiano  kati ya tasisi za uchaguzi vyombo vya ulinzi na usalama mitandao ya vijana na mashirika ya kiraia ili  kukuza ushiriki wa Amani na utulivu katika kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Sauti ya Mkurugenzi mkuu wa tasisi ya Pamoja Youth Initiative Rashid Mwinyi.

Nae mkuu wa kurugenzi ya huduma  za uchaguzi Khamis Issa Khamis amesema Tume ya Uchaguzi Zanzibar itaendelea kushirikiana na asasi mbalimbali za kiraia kwa lengo la kutoa elimu ya mpiga kura katika jamii sambamba na kudumisha Amani na utulivu nchini.

Sauti ya Mkuu wa kurugenzi ya huduma  za uchaguzi Khamis Issa Khamis.

Mdahalo huo n ni hatua muhimu kuelekea  kuimarisha misingi ya demokrasia Zanzibar  kupitia Amani  ushirikishwaji  na uwajibikaji wa pamoja.