Zenj FM

ZSSF yatoa mwongozo kwa Baraza la Mji Kati kuhusu viwanja vya watoto

18 April 2025, 4:29 pm

Maafisa kutoka Baraza la Mji Kati wakiwa na Wenyeji wao Maafisa wa ZSSF wakibadilishana uzowefu katika uendeshaji wa Viwanja vya Skukuu hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi za ZSSF Kilimani Zanzibar.

Baraza la mji Kati.

Baraza la Mji Kati wametakiwa kufuata taratibu, sheria na Kanuni zilizowekwa na Serikali pindi wanapotaka kuanzisha Viwanja vya kufurahia Watoto kwalengo la kuwa na Viwanja vilivyo bora.
Meneja Mipango kutoka ZSSF ambae pia Msimamizi wa Viwanja vya kufurahia Watoto Kariakoo Unguja Abdul Azizi Mohammed Ramia ameyasema hayo huko Ofisini kwake ZSSF Kilimani Mjini Zanzibar.
Amesema Baraza la Mji Kati watakapofuta Miongozo iliyowekwa watapata mafanikio makubwa na itapelekea kuongezeka kwa Mapato katika Baraza hilo na kufikia Malengo waliojiwekea.

Sauti ya Meneja Mipango ZSSF Abdul Azizi Mohammed Ramia.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Baraza la Mji Kati Rehema Khamis Hassan amesema lengo la kufika katika afisi za ZSSF ni kutaka kufahamu namna gani wanaendesha shughuli hizo pomoja na kujifunza mambo mbalimbali.

Sauti ya Kaimu Mkurugenzi Baraza la Mji Kati Rehema Khamis Hassan.

Nae Mkuu wa Divisheni ya Mapato Uchumi na Wajasiriamali wa Baraza hilo Helena John Bartholomeo ameahidi kuifanyia kazi elimu waliopatiwa kwa lengo la kurejesha haduma kwa Jamii pia kuongeza Mapato katika Baraza hilo

Sauti ya Mkuu wa Divisheni ya Mapato Uchumi na Wajasiriamali wa Baraza hilo Helena John.

Jumla ya Maafisa watano 5 Kutoka katika Kitengo cha Mapato, Mipango na Maendeleo ya Jamii Ofisi ya Baraza la Mji Kati wameshiriki katika Ziara hiyo.