Zenj FM

DC Kusini Unguja atoa onyo wanaojichukulia sheria mkononi

14 May 2024, 3:57 pm

Mkuu wa wilaya ya Kusini Unguja Cassian Galos Nyimbo akiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP. Daniel Emanuel Shillah, wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha Polisi Makunduchi. Picha na Omary Hassan

Na Omary Hassan

Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Cassian Galos Nyimbo amesema ujenzi wa vituo vipya vya Polisi nchini uendane na matumizi ya wananchi kutafuta haki kwa misingi ya sheria na kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi.

Akiweka jiwe la msingi Kituo cha Polisi Makunduchi huko Kijiji cha Makunduchi, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja Nyimbo amesema ni vyema wananchi kufuata sheria katika kupata haki zao.

Amesema  Wilaya ya Kusini Unguja imeanza kuwachukulia hatua na wahalifu wakiwemo wafanyabiashara ya mabaa  yanayofanya biashara na kupiga mziki bila ya kuwa na leseni.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Cassian Galos Nyimbo.

Nae Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP. Daniel Emanuel Shillah amesema kukamilika kwa ujenzi wa Jengo Jipya la Kituo hicho kilichogharimu Zaidi ya T.shs milioni 684,000,000/= kutaboresha utendaji wa Polisi katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Sauti ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP. Daniel Emanuel Shillah.