wananchi waungana kulima barabara za mtaa
Keifo FM

Wananchi waungana kulima barabara za mtaa

12/03/2026, 13:05

Wananchi wa ubalozi wa msasani kitongoji cha ipyana wakiendelea na shughuri ya kulima barabara

Wananchi wa ubalozi wa Msasani kitongoji cha Ipyana wilayani kyela wamehamasishana kulima barabara korofi kipindi hiki cha Mvua za masika na kupelekea kukosekana kwa mawasiliano kati ya ubalozi wao na balozi zingine.

Na Masud Maulid

Wananchi wa ubalozi wa msasani kitongoji cha ipyana a kata ya ipyana wilaya ya kyela wamejitokeza kushiriki zoezi la kujitolea kulima barabara iliyopo kwenye ubalozi huo kwa lengo la kurahisisha mawasiliano pamoja na kuepukana na maji kujaa kwenye makazi yao.

Akizungumza na mwandishi wa habari balozi wa eneo hilo Widley Mwasyika amaesema uamuzi wa wananchi kujitolea kufanya kazi hiyo  ni kutokana na changamoto ya ubovu wa barabara kutopitika wakati wa masika na  kupelekea maji kujaa kwenye makazi yao.

sauti ya balozi mwasyeka

Mwasyika ameongeza kuwa matengenezo hayo yatasaidia wenye viwanja pia kuuza kwa bei nzuri  kutokana na miundombinu kupitika,kurahisisha usafirishaji  mazao kutoka mashabani  pamoja na wananchi kwenda kupata huduma za kijamii nje ya ubalozi wao.

sauti ya balozi

Baadhi ya Wananchi wanaoshiriki zoezi hilo wamesema, moja ya sababu inayowahamasisha kushiriki kulima barabara ni kutokana na  maeneo ya ubalozi kupata shida kipindi cha masika maji kukosa mwelekeo na kujaa kwenye  makazi yao,huku Bernadi Nindi akiongeza kuwa,eneo hilo limekuwa changamoto  pia kwa watu wenye vyombo vya moto kuvipaki  mbali na makazi yao.

sauti ya wananchi

Eneo la Ubalozi wa Msasani kata ya Ipyana Wilaya ya Kyela awali lilitumika kwa shughuli za kilimo kabla ya kuanza kujenga  nyumba na sasa kuwa eneo la makazi.

0-0x0-0-0#