Keifo FM

Swebe: CCM acheni uoga CHADEMA tunawanyima usingizi

28 May 2024, 15:58

Pichani ni Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Kyela Victoria Swebe akiwa katika ofisi za chama hicho zilizopo hapa wilayani Kyela. Picha na Masoud Maulid

Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Kyela Victoria Swebe amekitaka Chama Cha Mapinduzi CCM kuacha uoga wa kiasiasa badala yake wajitokeze hadharani katika kuwahudumia wananchi.

Na Masoud Maulid

Saa chache baada ya Chama Cha Mapinduzi CCM Kyela kutangaza kuwapokea wanachama wapya kutoka CHADEMA, Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimekanusha taarifa za wanachama wake kata ya Kajunjumele kujiunga na CCM.

Katika taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Kyela Victoria Swebe amesema taarifa zinazoenezwa na viongozi wa CCM kuwapokea wanachama kumi na watano kutoka Chadema si za kweli na kuwa watu hao ni wanachama wa vyama vingine vya siasa na si CHADEMA.

Sauti ya victoria swebe akikanusha taarifa za CCM kuwapokea nwanachama wa Chadema kajunjumele

Swebe ameongeza kuwa hakuna mwanachama wa Chadema ambaye amehamia CCM kwa kuwa  wanachama wa CHADEMA  wapo imara na hata anayetajwa kujiunga na CCM amewahi kuwa kwenye vyama vingine vya upinzani ikiwemo NCCR-Mageuzi hivyo Chadema  haijapoteza wanachama kwa idadi ambayo imetajwa na viongozi wa CCM.

Sauti ya victoria Swebe aliyepokelewa ni mwanachama wa NCCR-Mageuzi
Pichani ni baadhi ya wajumbe wa chama hicho wakiongozwa na mwenyekiti wa BAZECHA wilaya ya Kyela Julius Minga kushoto kwake ni West Mwaseba wakimsikiliza mwenyekiti wa CHADEMA kyela Victoria Swebe

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo ameongeza kuwa,chama cha mapinduzi ni chama kikongwe hapa nchini Tanzania,hivyo viongozi wake waache uoga badala yake wafanye kazi za wananchi na si kujinadi juu ya kuvuna wanachama wa chadema ambapo matokeo yake ni kuipaisha chadema na kuonesha inawanyima usingizi muda wote.

Sauti ya victoria Swebe

Kuelekeza uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu hapa nchini Tanzania imekuwa ni kawaida kwa baadhi ya wanachama kutoka vyama mbalimbali kuhama vyama vyao na kujiunga na vyama vingine.