Zenj FM

Uchaguzi wa 2025 kuwa rafiki kwa watu wenye mahitaji maalum

4 September 2025, 5:09 pm

Mkuu wa Mkurugenzi wa Elimu ya Wapiga Kura na Mawasiliano kwa Umma wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Juma S. Sheha.

Na Mary Julius.

Mkuu wa Mkurugenzi wa Elimu ya Wapiga Kura na Mawasiliano kwa Umma wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Juma S. Sheha, amesema tume hiyo imejipanga kikamilifu kuhakikisha watu wenye mahitaji maalum wanashiriki ipasavyo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza na Zenji FM, Juma amesema ZEC imeandaa vitambulisho maalum kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum, wakiwemo watu wenye ulemavu, ili kuwapa kipaumbele wanapofika katika vituo vya kupigia kura.
Amesema Tume hiyo pia imeandaa kifaa maalum cha nukta nundu kwa ajili ya watu wenye changamoto ya uoni, ili kuwawezesha kupiga kura wao wenyewe bila kuhitaji msaada kutoka kwa mtu mwingine.

Sauti ya Mkurugenzi wa Elimu ya Wapiga Kura na Mawasiliano kwa Umma wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Juma S. Sheha.

Aidha,ameiomba jamii kutowaficha watu wenye ulemavu bali wawahimize kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchaguzi.

Sauti ya Mkurugenzi wa Elimu ya Wapiga Kura na Mawasiliano kwa Umma wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Juma S. Sheha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Jumuiya za Watu Wenye Ulemavu Zanzibar SHIJUWAZA, Ali Machano.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Jumuiya za Watu Wenye Ulemavu Zanzibar SHIJUWAZA, Ali Machano ametoa wito kwa watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi kwani haki ya kupiga kura ni haki ya kila raia wa Zanzibar.
Mkurugenzi Ali amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama vinadumishwa wakati wa uchaguzi mkuu.
Aidha Amesema Tume ya Uchaguzi ZEC pia imeweka mkakati wa kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira shirikishi na rafiki kwa watu wenye ulemavu,

Sauti ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Jumuiya za Watu Wenye Ulemavu Zanzibar SHIJUWAZA, Ali Machano.

Shirikisho la Jumuiya za Watu Wenye Ulemavu Zanzibar SHIJUWAZA limeandaaa majukwaa kwa ajili ya kuwahamasihsha watu wenye ulemavu kushiriki katika shughuli za kisiasa na uchaguz mkuu wa october 2025.