Zenj FM

ZEC yaanza rasmi zoezi la uchukuaji wa fomu za uteuzi Zanzibar

28 August 2025, 5:38 pm

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Thabit Idarous Faina.

Na Mary Julius.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Thabit Idarous Faina, ametangaza kuwa zoezi la uchukuaji wa fomu za uteuzi kwa ajili ya nafasi ya urais, uwakilishi, na udiwani limeanza rasmi leo.
Mkurugenzi Faina amesema kuwa zoezi hilo litaanza kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuchukua fomu ya nafasi ya urais mnamo Agosti 30, 2025, saa 4:00 asubuhi, katika ofisi za Tume ya Uchaguzi ZEC.

Sauti ya Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Thabit Idarous Faina.

Kwa wagombea wa nafasi za uwakilishi na udiwani, Mkurugenzi amesema watachukua fomu katika ofisi za wilaya, ambako maofisa wa jimbo wako tayari kutoa huduma.

Sauti ya Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Thabit Idarous Faina.

Aidha, Mkurugenzi amesema katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, Tume yanatarajia kutumia Shilingi bilioni 12 kwa ajili ya shughuli zote za uchaguzi.

Sauti ya Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, Thabit Idarous Faina.