Zenj FM

Wananchi watakiwa kufika mahakamani kutoa ushahidi

28 May 2024, 4:30 pm

Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Zubeir Chembera akizungumza katika kikao kazi kilichofanyika Makao Makuu ya Polisi Zanzibar .Picha na Omar Hassan

“Mnaosimamia upelelezi chukueni hatua kesi zipate mafanikio mahakamani” amesema D/DCI Chembera.

Na Omar Hassan / Said Bakar

Viongozi wanaosimamia Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika ngazi ya Mikoa, Wilaya na Vituo vya Polisi wametakiwa kuwasimamia wapelelezi kutimiza wajibu wao na kuwakamata mashahidi wanaoshindwa kufika kutoa ushahidi ili kesi zisishindwe kupata hatia Mahakamani.

Akizungumza na Wakuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mikoa, Wilaya na Vituo, huko Makao Makuu ya Polisi Zanzibar Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Zubeir Chembera amesema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya mashahidi kutofika kutoa ushahidi Mahakamani hali inayopelekea kesi kushindwa Mahakamani na Watuhumiwa wa Makosa mbalimbali kuachiwa huru.

Sauti ya Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Zubeir Chembera.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Polisi Omar Khamis Abdallah Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Kaskazini Unguja amewataka wananchi kuacha muhali na kuepuka kuzimaliza kesi kwa mapatano na badalayake kufika Mahakamani kutoa ushahidi ili lengo la kuekwa adhabu lifikiwe.

Sauti ya Kamishna Msaidizi wa Polisi Omar Khamis Abdallah.