Radio Jamii Kilosa

Wamiliki day care wilayani Kilosa watakiwa kusajili

17 June 2026, 08:52

Picha ni wamiliki wa day care pamoja na waratibu wa mradi wa Kinara Totocare.

Wadau wa shirika la Kinara lililopo Mkoani Morogoro wameendelea kuwaomba wamiliki wa shule za kulelea watoto wadogo (day care) kuendelea kusajili vituo vyao ili viweze kutambulika na mamlaka husika.

Na Aloycia Mhina

Wamiliki wa vituo vya shule za kulelea watoto wadogo mchana  ( day care ) Wilayani Kilosa wametakiwa kusajili vituo vyao ili kuendana na matakwa ya serikali.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Mratibu wa Day care Wilaya ya Kilosa Silvester Williamu Katikaza wakati akifunga mafunzo ya Wamiliki wa Vituo vya Day care  vilivyoko katika Kata ya Dumila Wilayani Kilosa.

Katikaza amewapongeza wadau wa Shirika la Kinara lililoko Morogoro kwa kuwapatia mafunzo Wamiliki hao ikiwemo kuwataka kusajili vituo ili kuendana na kasi ya Serikali.

Aidha amewataka kusajili watoto kuanzia umri wa miaka miwili hadi miaka minne kama mfumo unavyotaka wasipofanya hivyo watakuwa wanaenda kinyume na mfumo wa Serikali wa Kusajili Vituo hivyo vya Day Care .

Pichani ni William Katikata Mratibu wa shule za Daycare Wilaya ya Kilosa.

Sauti ya William Katikaza Mratibu wa day care Wilaya ya Kilosa

Kwa upande wake Mratibu wa mradi wa Kinara Toto Care  Prisca  Norbert amesema kuwa mafunzo hayo waliyoyapata yatawafikisha mbali na kuhakikisha vituo vinasajiliwa na kuwaomba Serikali kupitia ustawi wa Jamii washirikiane kwa pamoja, ambapo Salma Simbalyana kutoka Kinara Morogoro amewataka wamiliki kutumia mitandao ya Kijamii ili kutangaza Biashara zao ili  jamii wapate kuona wanachofanya.

Pichani ni Prisca Norbert Mratibu wa Kinara Totocare Mkoa wa Morogoro.

Sauti ya Prisca Norbert Mratibu wa mradi wa Kinara Toto care

Kwa upande wa Wamiliki wa Day care   Bi  Paulina  Ikhanga na  Rachel  Musa Baraja kwa kuwashukuru Ustawi wa Jamii na Wadau wa Mradi Kinara  Toto care shukuru kwa kupata mafunzo hayo kwani wamejifunza vitu vingi ikiwemo malezi na ulinzi wa mtoto, Lishe Bora na uzazi wa mpango.

Sauti za wamiliki wa shule za Day care