Pambazuko FM Radio
Pambazuko FM Radio
18 February 2026, 7:23 pm

Tukio hilo ni la kwanza kutokea katika kijiji hicho
Na David Ngogolo/Nicolatha Mpaka
Mtoto wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 15, mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Moonlight iliyopo kijiji cha madibila, kata ya Lupiro, Wilaya ya Ulanga amefariki dunia kwa madai ya kujinyonga kwa kutumia kamba za viatu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Golani Kijiji cha Madibila, Bw. Hamis Kambwili, akizungumza na Pambazuko FM kwa njia ya simu tukio hilo lilitokea Februari 16, 2026 majira ya saa mbili kamili usiku.
Aidha, amewasihi wazazi na jamii kwa ujumla kuwa karibu na watoto wao ili kubaini changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi mapema.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho, akiwemo Khadija Mayambua na Fadhili Rashid Hemed, wamesema wameshtushwa na tukio hilo kutokana na umri mdogo wa mtoto huyo.
Wananchi hao pia wamewataka wazazi na walezi kuwa na utamaduni wa kuzungumza na watoto mara kwa mara, kusikiliza matatizo yao na kuwapatia msaada unaostahili.
Hata hivyo Pambazuko FM inaendelea kufuatilia taarifa hii kwa mamlaka zinazohusika ili kujua chanzo cha tukio hilo.