Pambazuko FM Radio

TFS watambua mchango wa redio kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi Kilombero

13 February 2025, 9:38 pm

Na Katalina Liombechi

Wakala wa huduma za Misitu Tanzania TFS Wilaya ya Kilombero imesema kuwa Radio imekuwa na Mchango mkubwa katika kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia nchi.

Hayo ni kwa Mujibu wa Mhifadhi Daraja la Kwanza  Kutoka mamlaka hiyo Shukrani Madinda wakati akizungumza na Radio Pambazuko FM Ofisini kwake.

Mhifadhi huyo amesema kupitia radio wamekuwa wakielimisha jamii kuhusu shughuli za Uhifadhi hasa kutunza rasilimali misitu,kuelimisha njia mbadala za kiuchumi na Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ili kupunguza Uharibifu katika maeneo yaliyohifadhiwa ili kufanya maisha kuwa endelevu.

picha ya Mhifadhi Daraja la Kwanza  TFS Kilombero Shukrani Madinda(picha na Katalina Liombechi)
sauti ya Mhifadhi TFS Shukrani Madinda

Hata hivyo baadhi ya Wananchi Katika Mtaa wa Uwanja wa Taifa A Halmashauri ya Mji wa Ifakara wameelezea maoni yao juu ya Mchango wa Radio .

Sauti za baadhi ya wananchi Ifakara

Ikumbukwe kuwa Siku ya Radio Duniani huadhimishwa kila ifikapo February 13, ambapo kwa mwaka huu maadhimisho hayo yamebeba kauli mbiu ya “RADIO NA MABADILIKO YA TABIANCHI”