Pambazuko FM Radio

Kituo cha kupoza Umeme Ifakara kina ziada ya Megawati 11 zisizotumika

2 April 2026, 13:53

Picha ya kituo cha kupoza Umeme Ifakara{Picha na Kuruthum Mkata}

Uwepo wa kituo hicho umeondoa kwa kiasi kikubwa tatizo la kukatika kwa umeme katika maeneo ya Mng’eta na Mchombe, hivyo   REA kwa juhudi zake za kusambaza umeme vijijini na kuomba iongeze kasi katika maeneo mengine”-Meneja Mkuu wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kusini

Na Kuruthum Mkata

Kituo cha kupoza umeme Ifakara kina ziada ya megawati 11 ambazo bado hazijatumika licha ya kuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 18

 Hayo yameelezwa  na Meneja wa Miradi ya kusambaza Umeme kutoka REA Mhandisi Deogratius Nagu wakati wa ziara ya Jukwaa la Wahariri Nchini  walipotembelea kituo hicho kilichopo kata ya kibaoni halmashauri ya mji wa ifakara wilayani kilombero leo machi, 31 Ambapo amesema uwekezaji huu umeongeza upatikanaji wa umeme katika wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga.

Meneja wa Miradi ya kusambaza Umeme kutoka REA Mhandisi Deogratius Nagu{Picha na Kuruthum Mkata}

Sauti ya Meneja wa Miradi ya kusambaza Umeme kutoka REA Mhandisi Deogratius Nagu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Dunstan Kyobya, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi bilioni 25 zilizowezesha ujenzi wa kituo hicho huku  Akisema kuwa mradi huo umewanufaisha wananchi huku ukifungua fursa mpya za kiuchumi ikiwemo uanzishaji wa viwanda

Picha ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Dunstan Kyobya(Picha na Kuruthum Mkata)

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Dunstan Kyobya

Naye Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kusini Mhandisi Masingija Lugata amesema uwepo wa kituo hicho umeondoa kwa kiasi kikubwa tatizo la kukatika kwa umeme katika maeneo ya Mng’eta na Mchombe, hivyo  ameishukuru REA kwa juhudi zake za kusambaza umeme vijijini na kuomba iongeze kasi katika maeneo mengine

Sauti ya Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kusini Mhandisi Masingija Lugata

Aidha, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)Deogratius Balile ameipongeza REA kwa uwekezaji huo, akisema umechochea ukuaji wa fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kuanzishwa kwa viwanda.

Picha ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF)Deogratius Balile (Picha na Kuruthum Mkata)

Sauti ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF)Deogratius Balile