Pambazuko FM Radio

TARURA Kilombero yatoa ufafanuzi vifusi kuchelewa kusambazwa

11 February 2026, 8:29 pm

Picha ya moja ya barabara kifusi kiliwahi kukaa muda mrefu eneo la Kiyongwile A (Picha na Amina Mrisho)

Mkandarasi alipata changamoto ya vifaa kuharibika.

Na Amina Mrisho

Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) wilaya ya Kilombero umeeleza sababu za kuchelewa kusambaza vifusi katika barabara za halmashauri ya mji wa Ifakara.

Akizungumza na Pambazuko FM, Februari 9,2026 Meneja wa TARURA wilaya ya Kilombero,Mhandisi Sadiq Karume, amesema ucheleweshaji huo umetokana na kuharibika kwa baadhi ya vifaa wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Picha ya Meneja wa TARURA Kilombero Mhandisi Karume (Picha na Katalina Liombechi)
Sauti ya Meneja TARURA Kilombero

Aidha, amewataka wananchi kutunza miundombinu ya barabara.

Sauti ya Meneja TARURA Kilombero

Ikumbukwe kuwa mapema mwezi Januari, Pambazuko FM ilitembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Kiyongwile A ilijionea na wananchi walieleza changamoto wanazokumbana nazo kutokana na vifusi kuchelewa kusambazwa.

Sauti ya Mwananchi Kiyongwile