Pambazuko FM Radio
Pambazuko FM Radio
10 February 2026, 8:38 pm

“Baadhi ya wagonjwa wanaofika hospitalini wanadai wapo wengine mitaani lakini hawajapata ujasiri wa kujitokeza kutokana na mitazamo potofu”
Na Katalina Liombechi
Mratibu wa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi Kipaumbele katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Hamis Ngayungwa, ameitaka jamii kuacha imani potofu kuhusu ugonjwa wa mabusha na badala yake kufika hospitali kupata matibabu yanayotolewa bure.
Akizungumza na Pambazuko FM kuhusu kampeni ya upasuaji wa mabusha inayoendelea katika Kituo cha Afya Kibaoni tangu Januari 26, 2026, Ngayungwa amesema mwitikio bado si wa kuridhisha licha ya baadhi ya wananchi kujitokeza.
Kwa upande wao, baadhi ya wakazi wa Viwanjasitini wamewahimiza wagonjwa wa mabusha kujitokeza mapema kwa matibabu na kuachana na dhana zisizo na msingi.

Aidha Ngayungwa ameuelezea ugonjwa wa mabusha na chanzo chake.