Pambazuko FM Radio

10,424 wana maambukizi ya VVU Ifakara

30 November 2025, 4:40 pm

Picha ya Esther Mtweve Mratibu wa UKIMWI Ifakara ngazi ya jamii(Picha na Amina Mrisho)

“Tunapenda kuisisitiza jamii maambukizi bado yapo kwahiyo waendelee kuchukua tahadhari, tuondoe unyanyapaa na tuwajali wengine”

Na Amina Mrisho

Kadiri dunia inavyokaribia kuadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani tarehe 1 Desemba, jamii imeshauriwa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa kuwa bado vipo na vinaendelea kuathiri maisha ya watu.

Ushauri huo umetolewa na Mratibu wa Masuala ya UKIMWI ngazi ya jamii katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Bi. Esther Mtweve, alipokuwa akizungumza na Radio Pambazuko ofisini kwake.

Sauti ya Esther Mtweve Mratibu wa UMIMWI Ifakara ngazi ya Jamii

Kwa upande wake, Mratibu wa Masuala ya UKIMWI ngazi ya Hospitali, Dkt. Rajabu Chomboko, amesema kuwa katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuna jumla ya watu 10,424 wanaoishi na Virusi vya UKIMWI, ambapo wanaume ni 3,090 na wanawake ni 7,334.

Sauti ya Rajab Chomboko Mratibu wa UKIMWI Ifakara

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Ifakara (KONGA), Bi. Grace Mshana, amesema maadhimisho ya siku hiyo hutumika kukumbushana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mapambano dhidi ya UKIMWI.

Sauti ya Grace Mshana Mwenyekiti wa (KONGA)

Kauli mbiu ya siku ya Ukimwi Duniani kwa mwaka huu 2025 inasema: “Imarisha Mwitikio, Tokomeza UKIMWI.”