Pambazuko FM Radio

Wakulima watakiwa kuongeza thamani zao la mpunga

23 October 2025, 7:03 pm

Picha ya Emmanuel Kadilo Afisa Kilimo Ifakara(Picha na Isdory Mtunda)

Kwa kipindi kirefu wakulima katika bonde la kilombero wamekuwa wakiuza mpunga badala ya kuuza mchele kitu  ambacho haishauriwi kwani kufanya hivyo kunapunguza thamani ya zao hilo

Na Kuruthumu Mkata

Serikali kupitia Idara ya Kilimo Halmashauri ya Mji wa Ifakara imeendelea kufanya jitihada mbalimbali za kuongeza thamani la zao la mpunga ili kuhakikisha wakulima wanapata tija kupitia zao hilo.

Licha ya hatua ambazo zinachukuliwa baadhi ya wakulima wamekuwa wakiuza mpunga badala ya mchele ambao unakuwa na thamani na kipato kikubwa kama wanavyoeleza.

Sauti ya wakulima wanaouza Mpunga

Hata hivyo mmoja wa wakulima Ifakara amesema yeye huwa anauza mchele huku akiwataka wakulima wengine kubadili mtazamo,kuacha kuuza mpunga kwani kufanya hivyo kuna hasara kubwa.

Sauti ya Pascal Zakaria

Mmoja wa Wafanyabiashara wa Mchele Said Nakapala amesema kuna faida kubwa kuuza mchele huku akitoa wito kwa wakulima kuuza Mchele badala ya Mpunga.

Sauti ya Mfanyabiashara Mchele

Afisa Kilimo na pembejeo Halmashauri ya Mji wa Ifakara Emmanuel Kadilo akizungumza na Pambazuko FM Ofisini kwake amesema wamekuwa wakitoa elimu kwa wakulima kuzalisha kwa tija na kuongeza thamani ya zao la mpunga kwa kusindika na kupata bidhaa zingine itakayosaidia kumwongezea kipato.

Picha ya Emmanuel Kadilo Afisa Kilimo(Picha na Isdory Mtunda)