Pambazuko FM Radio

Huduma ugani yawapa changamoto wakulima

22 October 2025, 5:27 pm

Wananchi wa kijiji cha Mhelule wakipata elimu ya mbinu za kilimo bora; picha na; Isidory Mtunda

Wakulima wa kijiji cha Mhelule, kata ya Mwaya wilayani Kilombero wamelalamikia ukosefu wa msaada wa karibu kutoka kwa maafisa ugani, wakisema hawafiki mashambani kubaini changamoto zao. Maafisa wanasema idadi yao haitoshi kuwafikia wote, hivyo wakulima wanapaswa kuwafuata

Na: Isidory Mtunda

Baadhi ya wakulima wa kijiji cha Mhelule, kata ya Mwaya wilaya ya Kilombero, mkoa wa Morogoro, wamelalamika kutopata huduma ya karibu kutoka kwa maafisa ugani, wakisema hawatembelei mashamba yao ili kutambua changamoto wanazokutana nazo katika uzalishaji wa mazao.

wakulima wa kijiji cha Mhelule, wilaya ya Kilombero katika mafunzo ya mbinu za kilimo bora; Na; Isidory Mtunda

Malalamiko hayo yalitolewa jana wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwenye mafunzo maalum ya kilimo bora yaliyoendeshwa na kaimu afisa ugani wa kata ya Mwaya, Neema Mhongole.

sauti ya mkulima kijiji cha Mhelule

Akijibu hoja hiyo, Mhongole alisema, kwa kawaida mkulima ndiye anatakiwa kumfuata mtaalamu. Maafisa ugani ni wachache, na hivyo si rahisi kuwatembelea wakulima wote mmoja mmoja, hasa kama hawajaonyesha uhitaji. 

sauti ya kaimu afisa kilimo, Neema Mhongole

Wadau wa kilimo, Brown Kalambo na Jaliwa Jamson ambaye ni afisa masoko kutoka kampuni ya Meru Agrovet, walihimiza wakulima kufuata kanuni bora za kilimo na kuchukua tahadhari wanapotumia viuatilifu. 

afisa masoko wa kampuni ya Meru Agrovet, Jaliwa Jamson akitoa mada – Picha na: Isidory Mtunda

sauti za wadau wa kilimo; Kalambo & Jamson

Mafunzo hayo yalifanyika katika ofisi ya kijiji cha Mhelule kata ya Mwaya, Halmashauri ya mji wa Ifakara mkoani Morogoro na kuhudhuriwa na wakulima 166.