Pambazuko FM Radio

Flora aahidi kuwa mtetezi ‘mikopo kichefuchefu’

17 October 2025, 7:55 pm

Picha ya Baadhi ya wananchi katika uzinduzi wa kampeni(Picha na Nicolatha Mpaka)

“Naomba mnichague nitahakikisha watu wote wanapata mikopo bila kuonewa “

Na Katalina Liombechi

Mgombea Udiwani Kata ya Viwanjasitini kupitia Chama cha Mapinduzi Flora Kwangu leo akizindua Kampeni zake amesema miongoni mwa mambo atakayoshughulikia ni pamoja na changamoto ya Miundombinu ya barabara na kuwa sauti kwa wanawake wanaozalilishwa na mikopo kichefuchefu.

Kupitia hadhara hiyo katika Mkutano alioufanya Mtaa wa Minarani akiomba ridhaa ya kuchaguliwa kwa nafasi hiyo amesema hayo yanakwenda kufanyika kutokana na Ilani ya chama hicho ikigusa pia masuala ya elimu,Afya na uchumi wa watu.

Picha ya Flora Kwangu(Picha na Nicolatha Mpaka)
Sauti ya Flora Kwangu