Pambazuko FM Radio

Wanafunzi Mlimba wapata ujauzito, wakatisha masomo

25 September 2025, 9:49 pm

Picha ya Wanafunzi wa shule ya Sekondari Matundu Hill(Picha na Hija Namsa)

Jamii bado inahitajika kuchukua jukumu la ulinzi na uangalizi wa mtoto ili aweze kutimiza ndoto zake bila vikwazo

Na Hija namsa/Katalina Liombechi

Watoto wa kike wanne kati ya 67 wameshindwa kuhitimu Elimu ya Sekondari Katika shule ya Matundu hill iliyopo Kata ya Idete Halmashauri ya Mlimba,Mimba na utoro vikitajwa miongoni mwa sababu.

Katika mahafali ya 17 ya shule hiyo ambayo yamefanyika hii leo tarehe 25 Septemba, 2025 Mwalimu mkuu Isacka Kunyonga akisoma risala ya wanafunzi mbele ya Mgeni rasmi wadau na wazazi amesema  Jumla ya wanafunzi 99 kati yao wasichana 67 na wavulana 32 walitarajiwa kuhitimu masomo ya Sekondari kwa mwaka huu,lakini imekuwa tofauti ambapo idadi hiyo imepungua hadi kufikia 95 wasichana wakiwa 63 na wavulana 32 huku wengine wanne wa kike wakishindwa kuhitimu kutokana na mimba za utotoni,utoro na kuhama.

Picha ya Isacka Kunyonga Mwalimu Mkuu Matundu hill(Picha na Hija Namsa)
Sauti ya Isacka Kunyonga Mwalimu mkuu

Mgeni rasmi katika hafla hiyo Mhifadhi Zarina Sheweji Meneja kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Wilaya ya Kilombero alielezea kuguswa na jambo hilo na kutoa wito kwa wazazi na jamii kwa ujumla kuendelea kuwahimiza watoto wao hasa wa kike kupata elimu na kutoruhusu tabia hatarishi zinazopelekea kukatisha ndoto zao.

Picha ya Mhifadhi Zarina Sheweji Meneja wa TFS Kilombero(Picha na Hija Namsa)
Sauti ya Mhifadhi Zarina Sheweji

Katika hatua nyingine Mhifadhi zarina Katika hotuba yake, alionyesha kufurahishwa na juhudi kubwa ya kutunza mazingira ya shule hiyo hali iliyomfanya kuguswa na kuchangia maendeleo kwa kukabidhi kiasi cha Tsh.laki 2 na kuahidi kuunga mkono juhudi hizo kwa kuipatia shule miche 500 ya matunda kuendelea kuimarisha utunzaji wa mazingira pamoja na kuahidi kutoa mbao 50 kwa ajili ya kutengeneza meza na viti vya walimu hatua itakayosaidia kuwajengea walimu ari na mazingira bora ya kufundishia.

Sauti ya Mhifadhi Zarina Sheweji