Pambazuko FM Radio

Kilimo shadidi kuleta tija Kilombero

2 July 2025, 8:18 pm

Picha ya Kitalu mbegu ya Salu 5txd 306(Picha na Kuruthumu Mkata)

Kilimo shadidi ambacho kinatumia Mbegu kidogo,maji kidogo kinaleta kipato kikubwa na kuinua uchumi wa Mkulima

Na Kuruthumu Mkata

Taasisi inayojihusisha na Utafiti wa mbegu Tanzania TARI Ifakara waendelea kunufaisha jamii kwa kutoa elimu ya matumizi ya bora za kilimo za mpunga na kulima kisasa kwa kutumia teknolojia ya kilimo shadidi.

Hayo yaameelezwa leo Julai 2,2025 na Mtafiti wa mbegu bora za mpunga kutoka Taasisi hiyo Theodor Thomas wakati wa uzinduzi wa Siku ya Mkulima ambayo imefanyika katika Kijiji cha Katurukila kata ya Mkula Halmashauri ya Mji wa Ifakara ambapo pamoja na mambo mengine akizungumza mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya ameelezea historia ya mradi wa Kilimo hicho chenye tija kinachotumia mbegu kidogo,maji kidogo na mavuno mengi na kwamba inasaidia kupunguza hewa ukaa.

Sauti ya Theodor Thomas Kessy Mtafiti TARI

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstun kyobya Mgeni rasmi katika hafla hiyo amesema kwa kulima kisasa kutumia teknolojia hiyo ni wazi kuwa vijana watanufaika zaidi kutokana na kilimo shadidi kinajali mazingira na endelevu hivyo kusaidia kukua kiuchumi wakati huo mazingira yanabaki kuwa salama.

Picha ya DC Kyobya(Picha na Kuruthumu Mkata)
Sauti ya Dc Kyobya

Kwa upande wa wananchi wa kijiji cha Katurukila ambao wameonyesha nia ya dhati kulima kilimo hicho wameishukuru TARI kwa elimu waliyopatiwa juu ya kilimo shadidi huku wakitarajia kuondokana na hali ya umasikini na kwamba wataiambukiza elimu hiyo kwa wananchi wenzao.

Picha ya baadhi ya wananchi wa Katurukila na Watafiti wa TARI(Picha na Kuruthumu Mkata)

Mmoja wa wakulima wa Mfano salum ally ambaye pia mwenyekiti wa Kijiji hicho ameelezea kunufaika kupitia kilimo hicho na kwamba amekuwa akijivunia elimu anayoipata kutoka TARI.

Sauti ya Mkulima wa Mfano