Pambazuko FM Radio

Ndoto za vijana zinavyoishia njiani kwa kujihusisha na wizi mtandaoni

28 May 2025, 7:23 pm

Picha ya Selestine Luhungu mkazi wa Ifakara(Picha na Katalina Liombechi)

Inaelezwa kuwa ndoto za vijana vimekuwa zikiishia njiani kutokana na kujihusisha na wizi wa mtandaoni

Na Katalina Liombechi na David Ngogolo

Katika wakati huu ambao teknolojia imeleta fursa ya matumizi mbalimbali watu wengi hasa vijana wamekuwa wakitumia fursa nyingi za mtandaoni kibiashara na kujiendeleza kwa masuala mbalimbali lakini imemekuwa hatari kwa baadhi yao kwa wale wanaoingia tamaa ya mafanikio ya haraka kwa kudadisi mambo yanayopelekea kujikuta wakiingia kwenye Makosa ya Kimtandao (cybercrime).

Karibu kusikiliza makala kuhusu ndoto za vijana zinavyoishia njiani kwa kujihusisha na wizi wa mtandaoni ambapo utawasikia baadhi ya wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Ofisa wa TCRA na Mkuu wa Jeshi la polisi Wilaya ya Kilombero.

“Kama wanakilombero tukisema uhalifu huu basi inawezekana tunapata fedheha kama wilaya hii sio sifa nzuri” Amesema Daud Nkuba Mkuu wa Jeshi la Polisi Kilombero.