Pambazuko FM Radio
Pambazuko FM Radio
24 May 2025, 1:57 pm

Kupanda miti katika eneo hilo ni jitihada za kuhakikisha kuwa Mto Lumemo unasalia kuwa chanzo safi na salama kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Na Katalina Liombechi
Katika jitihada za kutunza mazingira na kulinda vyanzo vya maji wananchi wa Kata ya Viwanjasitini leo wamepanda miti 2,000 katika eneo la Mtaa wa Minarani kando ya Mto Lumemo.
Akizungumza katika zoezi hilo leo Mei 24,2025 Mtendaji wa Kata hiyo, Bi Hawa Ndachuwa amesema kuwa lengo kuu ni kuhifadhi chanzo hicho muhimu cha maji na kuimarisha hali ya mazingira katika eneo hilo.

Mbali na zoezi la upandaji miti, Afisa Mtendaji huyo pia alitumia mkusanyiko huo kuwakumbusha wazazi na walezi kuhusu wajibu wao wa malezi bora kwa watoto, akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha usalama na ulinzi wa watoto katika jamii.
Licha ya ‘ubize’ na shughuli za kujitafutia kipato tusisahau jukumu la malezi ya watoto wetu.
Wananchi walioshiriki waliipongeza ofisi ya kata kwa jitihada hizo, wakiahidi kuendeleza utunzaji wa miti iliyopandwa na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kimazingira.
