Pambazuko FM Radio

Six rivers Africa yawakumbuka watu 114 wenye uhitaji kwa kuwapatia kadi za bima za Afya za matibabu- katindiuka

16 October 2024, 4:08 pm

Wananchi Katindiuka katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara wakisubiri kupatiwa kadi za biama ya Afya [chf]iliyoboreshwa {Picha na Elias Maganga]

”Tunawashukuru sana Six River Africa kwa kutupatia msaada wa kadi za bima ya afya bure huu ni msaada kwetu ni mkubwa unapozungumzia uhai wa binadamu kwanza uwe na afya njema hawa ndugu zetu wameona mbali sana tunawashukuru”-wanufaika

Na Elias Maganga

Jumla ya watu 114 katika kaya 19 kata yakatindiukaKATIKA Halmashauri ya Mji wa Ifakara  wamepatiwa kadi za bima za afya CHF iliyoboreshwa   na shirika la six Rivers Africa

Awali akitoa maelezo ya bima hiyo,zilizotolewa oct 15 mwaka huu Elia matangila ni Afisa mwandikishaji wa bimaya CHF  iliyoboreshwaamesema inaanza kufanyakazi baaada ya siku saba kupita tangu kupatiwa kwa bima hiyo na lazima mgonjwa aanzie a zahanati na endapo atapatiwa rufaa aa bima hiyo itaendelea kutumika

Elia matangila ni Afisa mwandikishaji wa bima ya CHF  iliyoboreshwa{Picha na Elias Maganga]

Sauti ya Elia matangila ni Afisa mwandikishaji wa bima ya CHF  iliyoboreshwa

Naye afisa maendeleo ya Jamii kata ya Katindiuka Milka Pondo  amesema kaya 19 zilizochaguliwa ambazo hazifadhiliwi na mradi wowowte lakini zinaonekana zina uhitaji

Sauti ya fisa maendeleo ya Jamii kata ya Katindiuka Milka Pondo

Akizungumza wakati akikabidhi kadi hizo kwa wanufaika Diwani wa kata ya Katindiuka Tatu wakati Njayaga amelishukuru shirika la six rivers Africa kwa msaada huo na misaaada mbalimbali ambayo wameitoa kwa wakazi wa Katindiuka

Picha ya Diwani wa kata ya Katindiuka Tatu wakati Njayaga akigawa kadi za bima ya afya kwa wanufaika Katindiuka{picha na Elias Maganga]

Sauti ya Diwani wa kata ya Katindiuka Tatu wakati Njayaga

Baadhi ya wanufaika akiwemo Paschal Mabukula ameshukuru kitendo cha kupewa kadi ya bima ya afya ya CHF bure bila malipo ,kwani kabla ya kupatiwa bima hiyo pindi akipata matatizo ya kiafya humlazimu atafute hela ili akapate matibabu tofauti na sasa hata asipokuwa na hela bima hiyo itamsaidia naamewaomba waomba wadau wengine kuiga mfano wa six rivers Africa

Sauti za baadhi ya wanufaika wa bima ya afya akiwemo Mzee Paschal Mabukula

Kwa mujibu wa Afisa  mradi wa kuboresha watu na wanyama kuishi pamoja kutoka shirika la six Rivers Africa Irene Masonda amesema katika mpango huo kila kijiji wamechukuwa kaya 19pamoja na wategemezi wao watu sita .

Amesema kaya hizo duni  zimepatikana kwa ushirikiano kutka kwa wawezeshaji wao kwa kushirikiana na viongozi waliopo katika maeneo yao.

Sauti ya Afisa  mradi wa kuboresha watu na wanyama kuishi pamoja kutoka shirika la six Rivers Africa Irene Masonda

Zoezi hilo la uandikishaji wa biama za afya linaanza rasmi oct15 katindiuka hadi oct 27 litahitimishwa Kijiji cha Miwangani