Pambazuko FM Radio

Wananchi Kilombero jitokezeni kujiandikisha kupiga kura –Dc Kyobya

11 October 2024, 2:00 pm

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya akiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara Zahra Michuziwakiahamasisha zoezi la uandikishaji{Mpich na Kuruthum Mkata}

”Mwananchi atakayejiandikisha kwenye Daftari atapata fursa ya kupiga kura kuchagua au kuchaguliwa na yule ambaye hatajiandikisha hatoshiriki ucahguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Nov 27 mwaka huu” -Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya

Na Elias Maganga

Mkuuwa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya amewaongozana na  kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya na wananchi kwa ujumla katika zoezi la kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura lililoanza rasmi hii leo 11oktoba hadi 20 oktoba mwaka huu.

Picha ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya akijiandikisha kwenye kituo ca chekechea kitongoji cha Bomani [Picha na Kuruthum Mkata}

Akijiandikisha kwenye kitongoji cha bomani kilichopo Kijiji cha Kibaoni katika Halmahsauri ya Mji wa Ifakara Mkuu wa Wialaya Kyobya ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Kilombero kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha kwani hiyo itamfanya mwananchi apige kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika nov 27 mwaka huu na kwa wale ambao hawatajiandikisha hawatapiga kura.

DC Kyobya amesema Wilaya ya Kilombero ina vitongoji 458 huku ifakara pekee kukiwa na vitongoji 214 na Halmashauri ya Mlimba ina vitongoji 244 hivyo kila mwananchi katika kitongoji chake mwenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea  ajitokeze kushiriki zoezi hilo muhimu la kujiandikisha  

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara Bi Zahra Michuzi amesema mwananchi atakapojiandikisha kwenye daftari la ukaazi atapata haki ya kuchagua ama kuchaguliwa kutokana na sifa zilizoainishwa na Tume ya Uchaguzi,lakini kujiandikisha huko si kwasababu tu ya uchaguzi lakini pia kuisaidia serikali kupanga mipango yake ya baadae ya kujua idadi mahususi ya watu katika eneo husika na huduma za kijamii wanazozihitaji.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara Bi Zahra Michuzi{Picha na Kuruthum Mkata}
Sauti ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara Bi Zahra Michuzi

Kwa upande wao Sophia Mlela mwenyekiti wa Kitongoji cha Bomani na Frencesianus Zakaria Waya Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibaoni wamesema wananchi wamejitokeza na wanaendelea kujitokeza kujiandikisha na kadri siku zinavyoendelea wanaamini watafikia malengo ya uandikishaji.huku wakiwaomba wananchi kujitokeza wasisubiri siku ya mwisho wani siku hiyo watu watakuwa wengi na wengine wanaweza wakakosa kujiandikisha.

Sauti za Sophia Mlela mwenyekiti wa Kitongoji cha Bomani na Frencesianus Zakaria Waya Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibaoni

Nao baadhi ya wanananchi waliojitokeza kujiandikisha katika kituo cha chekechea kilichopo kitongoji cha Bomani Fidelis severine na Fida Enock Msola wametoa wito kwa wananchi kujitokeza kujiandikisha kwani wao tayari wameshajiandikisha

Sauti za baadhi ya wanananchi waliojitokeza kujiandikisha katika kituo cha chekechea kilichopo kitongoji cha Bomani Fidelis severine na Fida Enock Msola