Boma Hai FM

Wakabidhi jengo la baba, mama na mtoto Hai

6 March 2026, 4:33 pm

Pichani ni Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Hai Dionis Myinga(aliyevaa shati la drafti) akizindua jengo la baba mama na mtoto katika zahanati ya Nkweshoo.(picha na Salma Mgosso)

Katika kuendelea kuboresha huduma za afya hapa nchini wadau wa maendeleo kutoka taasisi ya Tumbili Foundation kwa kushirikiana na Holcim Foundation kutoka nchini Switzerland wamejenga jengo la baba, mama na mtoto katika zahanati ya Nkweshoo na kulikabidhi kwa serikali.

Na Elizabeth Mafie &Salma Mgosso
Hai – Kilimanjaro

Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miradi ya elimu, afya na miundombinu ya barabara katika wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha maisha ya wananchi ambapo wilaya ya Hai imepatiwa zaidi ya shilingi bilioni thelathini tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingia madarakani.

Pichani ni wananchi wa kata ya Machame Mashariki wakiwa katika hafla ya kukabidhiwa jengo hilo(picha na Elizabeth Mafie)
Pichani ni diwani wa kata ya Machame Mashariki Jordan Ngowi akiwa katika hafla ya kukabidhiwa kwa jengo hilo(picha na Elizabeth Mafie)

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hai Dionis Myinga, Machi 5, 2026 alipokuwa katika hafla ya kukabidhiwa jengo la baba, mama na mtoto katika zahanati ya Nkweshoo iliyopo kijiji cha Nkuu Ndoo kata ya Machame Mashariki.

Jengo hilo limejengwa na wadau wa maendeleo Tumbili Foundation kwa kushirikiana na Holcim Foundation kutoka nchini Switzerland, ambapo ujenzi wake umegharimu shilingi milioni mia moja arobaini.

Pichani ni mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Hai Dionis Myinga katika hafla ya kukabidhiwa jengo la baba, mama na mtoto katika zahanati ya Nkweshoo(picha na Elizabeth Mafie)
Pichani ni Stephan Manimo na mumewe ambao ni waanzilishi wa Tumbili Foundation wakisoma taarifa ya mradi(picha na Elizabeth Mafie)

Myinga amesema wafadhili wa mradi huo wamefanya kazi nzuri kwani mradi huo unagusa maisha ya wananchi moja kwa moja kwa kuboresha huduma za afya katika kata ya Machame Mashariki na kwamba wadau wengine wa maendeleo waendelee kujitokeza na kushirikiana na serikali kutekeleza miradi inayogusa maisha ya wananchi.

Sauti ya mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Hai Dionis Myinga.

Akisoma taarifa ya mradi mwanzilishi wa Tumbili Foundation, Stephan Manimo, amesema taasisi hiyo itaendelea kusaidia na kuunga mkono miradi ya maendeleo nchini na kwamba taasisi hiyo ina utaratibu wa kipekee ambapo kila safari wanayoandaa huzalisha rasilimali zinazosaidia kutekeleza miradi yenye manufaa kwa jamii.

Sauti ya mwanzilishi wa Tumbili Foundation Stephan Manimo

Kwa upande wake diwani wa kata ya Machame Mashariki Jordan Ngowi, amewashukuru wadau hao wa maendeleo kwa kutekeleza mradi huo akisema kuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi wa eneo hilo ambao hapo awali walilazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Sauti ya diwani kata ya Machame Mashariki Jordan Ngowi

Nao wananchi wa kijiji cha Nkweshoo katika kata ya Machame Mashariki wamesema kuwa ujenzi wa jengo hilo utawasaidia kupata huduma za afya karibu na kwa wakati.

Sauti za wananchi wa kata ya Machame Mashariki wakieleza jinsi mradi huo utakavyowasaidia.