Boma Hai FM

Rutaraka asisitiza madiwani uwajibikaji na usimamizi wa miradi

26 January 2026, 2:36 pm

Pichani ni mwenyekiti Halmashauri ya wilaya ya Hai Edmund Rutaraka (katikati)(picha na Juma Robert)

Madiwani wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro wamehimizwa kusimamia kwa karibu shughuli za serikali za mitaa ili kuhakikisha uwajibikaji na matumizi sahihi ya rasilimali za umma ,Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Edmund Rutaraka, wakati akifunga mafunzo ya madiwani yaliyofanyika kwa siku mbili, huku akisisitiza usimamizi wa miradi na fedha za maendeleo.

Na Juma Robert Hai – Kilimanjaro

Madiwani wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuhakikisha wanasimamia vyema uendeshaji wa shughuli za serikali za mtaa katika halmashauri ya wilaya ya Hai ili kujenga halmashauri yenye hati safi kwa kipindi chote cha miaka mitano.

Pichani ni makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Trael Mboya (picha na Juma Robert)

Hayo yameainishwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai, Edmund Rutaraka wakati akifunga rasmi mafunzo ya madiwani yaliyofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Halmashauri ya Hai.

Pichani ni baadhi ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Hai (picha na Juma Robert)

Rutaraka amesema mafunzo hayo yatawasaidia madiwani kufahamu majukumu yao kikamilifu na namna ya kusimamia utekelezaji wake, ikiwa ni pamoja na kusimamia vyema fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi mbalimbali katika kata zao.

Sauti ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Edmund Rutaraka

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Masama Kusini Cedric Pangani, amesema mafunzo hayo yamekuwa chachu ya kujenga uelewa wa pamoja kuhusu nafasi ya madiwani katika kuimarisha demokrasia ya ndani na mahusiano bora na wananchi.

Sauti ya diwani wa kata ya Masama Kusini Cedrick Pangani.

 Amesema mafunzo hayo pia yanalenga kuwajulisha wananchi kuhusu uwajibikaji wa mabalozi wa mtaa, kwa kuhakikisha wananchi wanatoa taarifa za wageni wanaoingia kwenye mtaa ili kujulikana katika kaya husika na kuimarisha usalama wa wananchi wa mtaa au kata husika.

Sauti ya diwani wa kata ya Masama Kusini Cedrick Pangani.