Boma Hai FM

EAGMA yapandishwa kilele cha mlima Kilimanjaro

19 July 2025, 9:01 am

Mkurugenzi wa tuzo za East Africa Gospel Music Awards (EAGMA)  Magreth Chacha pamoja na wadau mbalimbali wakiwa katika geti la Marangu kwa ajili ya kupandisha tuzo hiyo katika kilele cha mlima Kilimanjaro.(picha na Salma Sephu)

Katika kuendelea kumtukuza Mungu kupitia muziki wa injili mkurugenzi wa tuzo za East Africa Gospel Music Awards apandisha tuzo hiyo kilele cha mlima Kilimanjaro.

Na Elizabeth Noel.

Moshi -Kilimanjaro

Tuzo ya Afrika Mashariki ya Muziki wa injili ( East Africa Gospel Music Awards( EAGMA  )imepandishwa Katika Kilele Cha Mlima Kilimanjaro kupitia Geti la Marangu lililopo Wilaya ya Moshi Vijijini  Mkoani Kilimanjaro .

Mkurugenzi wa tuzo za East Africa Gospel Music Awards (EAGMA)  Magreth Chacha

Akizungumza kwa Njia ya simu mkurugenzi wa tuzo za East Africa Gospel Music Awards (EAGMA)  Magreth Chacha amesema lengo la tuzo hiyo kupandishwa  mlima Kilimanjaro ni kwaajili ya Utukufu kwa Mungu na kuuheshimisha Muziki wa injili.

Sauti ya Mkurugenzi wa tuzo za East Africa Gospel Music Awards (EAGMA)  Magreth Chacha

Tuzo hiyo inatarajiwa Kufikishwa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro na kushushwa siku ya jumamosi ya Julai 19,2025 huku mgeni rasmi katika mapokezi ya tuzo hiyo akitarajiwa kuwa Askofu Fredrick Shoo