Boma Hai FM

Bweni la Machame sekondari kukamilika ndani ya siku 19

29 May 2025, 2:18 pm

Pichani ni bweni la shule wa wasichana Machame sekondari likiwa katika hatua za mwisho za ujenzi(picha na Faraja Ulomi)

Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wananfunzi kote na nchini,hii inaadhihirika wazi kutokana na miradi mbalimbali ya ujenzi inayoendelea huko mashuleni ikiwemo shule ya wasichana Machame.

Na Faraja Ulomi. Hai -Kilimanjaro

Afisa elimu  taaluma sekondari wilaya ya Hai Mkoa wa Kilimanjaro Bi Stella Mwangomale amesema kuwa mradi wa bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari ya wasichana Machame upo katika hatua nzuri  na kwamba mradi huo utakamalika ndani ya siku kumi na tisa.

Stella ameyasema hayo Leo Mei 29,2025 alipofika shuleni hapo Kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bweni hilo.

Pichani ni afisa elimu taaluma sekondari wilaya ya Hai Stella Mwangomale(picha na Faraja Ulomi)

Amesema kutokana na kazi kufanyika kwa haraka  imepelekea kufika hatua ya ukamilishaji  na kwamba baada ya kukamilika mradi huo utakabidhiwa.

“Tunaamini kabisa katika siku hizi zilizobakia,zimebaki siku 19 , na kazi inavyoonekana itamalizika hata kabla ya hizo siku 19, na itamalizika salama”Amesema Stella Mwangomale.

Sauti ya afisa elimu taaluma sekondari wilaya ya Hai Stella Mwangomale.

Kwa upande wake makamu mkuu wa shule ya  wasichana Machame  sekondari  Devartusi Swai akatoa shukrani zake kwa serikali Kwa kupeleka fedha kwa ajili ya mradi huo.

“Awali ya yote niishukuru serikali kwa ajili ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya bweni hili”Amesema Swai.

Sauti ya makamu mkuu wa shule ya wasichana Machame sekondari Devartusi Swai.