Boma Hai FM

Mwenge wa Uhuru kuzindua daraja la upinde wa mawe Siha

25 May 2025, 8:49 am

Daraja la upinde wa mawe lililopo kijiji cha Donyomurwa kata ya Donyomurwa wilayani Siha mkoani Kilimanjaro(picha na Bahati Chume)

“Ni kweli Mradi huu tunategemea utazinduliwa na mbio za  mwenge  wa uhuru mwaka huu, tunaishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kuleta mradi huu kwa  kushirikiana na wananchi wa Donyomurwa “

Na Elizabeth Mafie- Siha Kilimanjaro

Ujenzi wa daraja la upinde wa mawe llilopo Kijijii cha Donyomurwa kata Donyomurwa Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro limefikia asilimia 98  kukamilika na linatarajiwa kuzinduliwa na mbio za  Mwenge wa Uhuru Julai 2025.

Haya yamesemwa na Diwani wa Kata hiyo Lwitte Ndossi ,alipotembea Daraja hilo kwa lengo la kukagua  maendeleao ya ujenzi ambapo amesema hadi kukamika litagharimu zaidi ya milioni mia tatu.

“Ni kweli Mradi huu tunategemea utazinduliwa na mbio za  mwenge  wa uhuru mwaka huu, tunaishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kuleta mradi huu kwa  kushirikiana na wananchi wa Donyomurwa “amesema Ndosi

Sauti ya Diwani wa kata ya Donyomurwa Lwitte Ndossi.

Ndossi,amesema mradi huo utaondoa changamoto za muda mrefu katika eneo hilo kwani wananchi wamekuwa wakipitia changamoto mbalimbali  ikiwemo kusombwa na maji  na hata wakati mwingine kufariki dunia wakati wakivuka upande wa pili kufuata huduma mbalimbali za kijamii.

Diwani wa kata ya Donyomurwa Lwitte Ndossi.(picha na Bahati Chume)

 Ameeleza kuwa  zaidi ya  wananchi elfu tatu  wa vijiji vya loiwa ,Embokoi, Donyomurwa wataondokana na chanagmoto hiyo,  na kwamba daraja hilo ni kuiganishi cha mawasiliano na kijijii cha Mungushi kilichopo Wilaya Hai.

Mwenyekiti wa kijijii cha Donyomurwa Meshack Laizer amesema kukamilika kwa Mradi huo kutusaidia kuondoka adha ya wanafunzi wanaosoma shule ya msingi Kwamankuu kushindwa kwenda shule hasa kipindi cha mvua  hivyo kushindwa kupata masomo kwa ukamilifu.

Sauti ya mwenyekiti wa Donyomurwa Meshack Laizer.

Peter Laizer moja ya Wananchi hao  wamesema kukamilika kwa mradi huo ,kutachangia ukuaji wa uchumi katika hilo,na kupunguza gharama na muda wa safari.

 Mwananchi huyo akapata wasaa wa kumshukuru Rais Dkt  Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka  fedha kwenye mradi huo “ ameonyesha anatujali, hatuna budi ya kusema asante pia mbunge wetu wa jimbo Godwin Mollel pamoja na diwani wa kata tunawapa shukurani” Amesema Piter Laizer.

Sauti ya mwananchi wa kata ya Donyomurwa Piter Laizer.