Pambazuko FM Radio

Polisi Kilombero wafanya matendo ya huruma

12 February 2026, 8:21 pm

Picha ya Kamanda Nkuba na maofisa wengine wa Polisi walipomtembelea Mama wa watoto watatu(Picha na Katalina Liombechi)

Pamoja na mambo mengine Jeshi la Polisi limeendelea kuikumbusha jamii kutotelekeza familia zao kwani hali hiyo inaathiri malezi ya watoto

Na Katalina Liombechi

Katika kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi “Police Family Day” yanayofanyika Februari 13, kila mwaka, Jeshi la Polisi Wilaya ya Kilombero leo limefanya matendo ya huruma kwa kumtembelea mama mwenye watoto mapacha watatu aliyetelekezwa na mumewe katika eneo la Mahutanga, Kata ya Lumemo.

Jeshi hilo limemkabidhi msaada wa chakula pamoja na vifaa vya ujenzi (mchanga na saruji) kwa ajili ya kuboresha makazi yake ambapo pamoja na mambo mengine Jeshi la Polisi limeendelea kuikumbusha jamii kutotelekeza familia zao kwani hali hiyo inaathiri malezi ya watoto.

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kilombero, OCD Daud Nkuba, amesema ni utamaduni wa Jeshi la Polisi kuwa karibu na jamii kwa kushirikiana katika ulinzi na usalama pamoja na kufarijiana katika nyakati za mahitaji.

Aidha, familia ya Polisi Kilombero imemtembelea na kumfariji mtumishi mwenzao, Afande Julius, aliyekuwa akiugua, na kumpatia msaada wa mahitaji ya chakula.

Picha ya Kamanda Nkuba kulia akiwa na Afisa aliyekuwa akiugua waliyemtembelea Afande Julius(Picha na Katalina Liombechi)
Sauti ya Kamanda Nkuba

Christina Lishela mama wa mapacha watatu ,Diwani wa kata ya Lumemo pamoja mwananchi wa eneo hilo wameelezea kushukuru kwa msaada uliotolewa na jeshi la polisi kwa wahitaji huku wakiahidi kulipa ushirikiano Jeshi hilo katika masuala ya ulinzi na usalama.

Picha ya Bi Christina Lishela mama wa Mapacha watatu(Picha na Katalina Liombechi)
Sauti za Christina Lishela,Diwani na Mwananchi Kata ya Lumemo(Picha na Katalina Liombechi)

Maadhimisho ya Police Family Day hufanyika kila mwaka Februari 13 ambapo  Kwa mwaka 2026, yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Polisi Jamii, Rejesha Amani na Utulivu”, na katika Wilaya ya Kilombero yanatarajiwa kufanyika katika Viwanja vya Kiungani.”