Pambazuko FM Radio

EDO yamsifu mfadhili kutimiza ahadi ya kumsaidia binti yatima

16 October 2025, 6:52 pm

Picha ya Binti Maria Paula katikati akiwa na viongozi wa EDO(Picha na Nicolatha Mpaka)

“Tuone ya kwamba mtoto wa mwenzako ni wako unaweza kumpa msaada”

Na Nicolatha Mpaka

Uongozi wa Shirika la Enlighten Development Organiozation EDO linalopatikana Ifakara Morogoro umempongeza Bw. Zeno Kakweche kwa kutimiza ahadi yake ya kumnunulia mashine ya kushonea binti Maria Paula, mhitimu wa kituo cha EDO.

Bw. Zeno alitoa ahadi hiyo tarehe 14 Oktoba mwaka huu, wakati wa mahafali ya kituo hicho, na leo ametekeleza kwa vitendo kwa kumkabidhi rasmi cherehani hiyo mbele ya viongozi wa shirika.

Picha ya Bwana Kakweche akikabidhi Cherehani(Picha na Nicolatha Mpaka)
Sauti ya Kakweche

Mkurugenzi Mwenza wa EDO, Bi. Josephine Saidi, amesema wametambua moyo wa upendo wa Bw. Zeno na kupongeza hatua hiyo iliyotolewa mapema kuliko walivyotarajia.

Sauti ya Mkurugenzi Mwenza EDO

Kwa upande wake, mlezi wa kituo cha St. Laurenti, Bi. Rose Laurenti Njige, ameishukuru EDO na mfadhili huyo kwa kusaidia kutimiza ndoto za binti huyo anayelelewa kituoni hapo.

Sauti ya Mlezi kituo cha Watoto yatima St.Laurent

Maria Paula mwenyewe ameonyesha furaha na kutoa wito kwa vijana wenzake kutokata tamaa, bali kupambana ili kufikia ndoto zao.

Sauti ya Maria Paula