Pambazuko FM Radio

CRDB yagusa kwenye upungufu viti na meza 184 Ifakara

11 October 2025, 10:06 am

Picha ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Mahutanga(Picha na Kuruthumu Mkata)

Benki ya CRDB ina asilimia 1 kwa ajili ya jamii kuchangia maendeleo ya serikali

Na Katalina Liombechi

Katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja Benki ya CRDB imewajibika kwa kukabidhi Viti na Meza 50 katika shule ya Sekondari Mahutanga Halmashauri ya Mji wa Ifakara ikiwa ni sehemu kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja.

Kwa mujibu wa Meneja wa Benki hiyo Kanda ya Kati Chabu Mishwaro amesema CRDB imekuwa na utaratibu wa kutoa asilimia moja kurejesha kwa jamii kuchangia maendeleo kwa kugusa sekta mbalimbali kupitia programu ya “keti jifunze” kwa lengo la kuhakikisha mwanafunzi anapata utulivu anapojifunza darasani kama walilivyofanya katika shule hiyo.

Picha ya Chabu Mishwaro Meneja CRDB Kanda ya Kati(Picha na Kuruthumu Mkata)
Sauti ya Chabu Mishwaro Meneja CRDB Kanda ya Kati

Mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo Oktoba 08,2025 Mkuu wa Wilaya ya Kilombero wakili Dunstan Kyobya ameishukuru benki hiyo kwa kuunga mkono jitihada za serikali licha ya kuwa bado kuna upungufu wa viti na meza zingine 184.

Picha ya DC Kyobya(Picha na Kuruthumu Mkata)

Sauti ya DC Kyobya

Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wamesema awali walikuwa wanapata changamoto ya wengine kukaa chini na kukaa wawili katika kiti kimoja hivyo kwa kupata viti na meza imepunguza adha hiyo.

Picha ya Wanafunzi Shule ya Sekondari Mahutanga(Picha na Kuruthumu Mkata)