Pambazuko FM Radio

Ripoti tathmini mradi wa FOLUR inapitiwa Ifakara

1 October 2025, 7:41 pm

Picha ya wataalamu kwenye kikao cha kupitia ripoti ya tathimini mradi wa FOLUR(Picha na Kuruthumu Mkata)

Mradi huu unatekelezwa katika Halmashauri ya Mlimba kwa gharama ya shilingi bilioni 6, huku kiasi kingine kikitekelezwa katika Wilaya mbili za Zanzibar

Na Katalina Liombechi/Kuruthumu Mkata

Kikao cha siku tatu cha uthibitishaji wa ripoti za tathmini ya mradi wa maboresho mifumo ya chakula, matumizi ya ardhi na urejeshaji wa mazingira (FOLUR)kimeanza leo katika mji wa Ifakara, Wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro.

Kikao hicho kimewakutanisha wadau kutoka kongani ya Kilombero pamoja na visiwani Zanzibar, kikilenga kupitia kwa pamoja ripoti za tathmini kabla ya utekelezaji kamili wa mradi huo wenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 18.

Waratibu wa mradi huo kutoka Halmashauri ya Mlimba Joseph Mgana na Miza Khamis upande wa Zanzibar wamesema kikao hicho ni muhimu kwa kuhakikisha kuwa ripoti zilizotolewa zinazingatia hali halisi ya mazingira ya utekelezaji, pamoja na kutoa fursa kwa wadau kutoa maoni na mapendekezo ya maboresho kabla ya hatua zinazofuata.

Picha ya Miza Khamis Mratibu mradi wa FOLUR Zanzibar(Picha na Kuruthumu Mkata)
Sauti ya Joseph Mgana na Miza Khamis waratibu Mradi wa FOLUR Mlimba na Zanzibar

Wanjara Mgahywa Mratibu mkuu Mtekelezaji Mradi huo Kitaifa kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii amesema katika kikao hicho wataalam na wadau watatoa michango kwenye tahmini na tafiti mbalimbali yanayohusu majukumu ya mradi ambayo yametekelezwa kwa mwaka jana katika maeneo yote ya mradi Mlimba katika Wilaya ya Kilombero na Zanzibar.

Picha ya Wanjara Mgahywa Mratibu Mradi wa FOLUR kitaifa(Picha na Kuruthumu Mkata)

Sauti ya Wanjara Mgahywa

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero Abrahamu Mwaikwila akifungua kikao hicho akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya amesema kikao hicho ni cha makusudi kufanyika kwa wadau sahihi ambapo amewataka kujadiliana kwa kina kuainisha changamoto na namna ya kwenda kutekeleza Mradi wa FOLUR kwa Ufasaha.

Picha ya Abrahamu Mwaikwila DAS Kilombero(Picha na Kuruthumu Mkata)
Sauti ya DAS Kilombero

Lengo kuu la mradi huo wa Miaka Mitano ni kuimarisha usalama wa chakula, kulinda mazingira, na kuhakikisha matumizi endelevu ya ardhi kwa manufaa ya jamii za sasa na vizazi vijavyo.