Pambazuko FM Radio

ACT Wazalendo Ulanga waeleza utaratibu uchukuaji fomu

18 July 2025, 2:17 pm

Picha ya Ally Omary Matwiku(Picha Kwa hisani ya bwana Matwiku)

Kwa anayetaka kutia nia ya Ubunge nafasi iko wazi hatuna shaka na mtu yeyote anayetaka kutia nia kupitia chama chetu

Na Kuruthumu Mkata

Chama cha ACT-Wazalendo wilayani Ulanga kimetangaza kuanza rasmi mchakato wa uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwa uchaguzi ujao.

Akizungumza na Redio Pambazuko FM kwa njia ya simu leo, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo wilaya ya Ulanga Ally Omary Matwiku amesema zoezi hilo litaanza Julai 25 hadi Agosti 10, 2025.

Ameeleza kuwa chama kinakaribisha wanachama wote wenye sifa kujitokeza kuchukua fomu kwa nafasi za ubunge na udiwani, akisisitiza umuhimu wa ushiriki mpana wa wanachama katika mchakato huo wa kidemokrasia.

Sauti ya Ally Matwiku Mwenyekiti ACT Wazalendo Ulanga